53-Mukhtasari Aqiydah Ya Muislamu: Je, Ipo bid'ah inayoitwa bid-‘atun-hasanah’ katika Dini?

 Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

53-Je, Ipo bid'ah inayoitwa bid-‘atun-hasanah’ katika Dini?

 

Hapana! Hakuna bid’atun-hasanah (uzushi mzuri) katika Dini.

 

 

الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ

Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni neema Yangu, na Nimekuridhieni Uislaam uwe Dini yenu. [Al-Maaidah: 3]

 

 

((إِيَّاكُمْ وَمُحْدَثَاتِ الْأُمُورِ، فَإِنَّ كُلَّ مُحْدَثَةٍ بِدْعَةٌ، وَكُلَّ بِدْعَةٍ ضَلَالَةٌ)) صحيح رواه أبو داود

((Jitahadharini na uzushi wa mambo, kwani kila uzushi ni bid'ah na kila bid'ah ni upotofu)) [Swahiyh - Abuu Daawuwd]

 

Share