24-Kitaab At-Tawhiyd: Kuhusu Uchawi

Mlango Wa 24

بَابُ مَا جَاءَ فِي اَلسِّحْرِ

Kuhusu Uchawi


 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

 Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

وَلَقَدْ عَلِمُوا لَمَنِ اشْتَرَاهُ مَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ۚ

((na kwa yakini walijua kwamba atakayechuma haya hatopata katika Aakhirah fungu lolote)) [Al-Baqarah (2: 102)]

 وَقَوْلِهِ:

 Na kauli Yake:

يُؤْمِنُونَ بِالْجِبْتِ وَالطَّاغُوتِ

((Wanaamini itikadi potofu na twaghuti))  [An-Nisaa (5: 51)]

 

 قَالَ عُمَرُ : الْجِبْتُ اَلسِّحْرُ، وَالطَّاغُوتُ اَلشَّيْطَانُ

‘Umar  (رضي الله عنه) amesema: Al-Jibti ni uchawi na Atw-Twaaghuwt ni shaytwaan.

 

 وَقَالَ جَابِرٌ: اَلطَّوَاغِيتُ كُهَّانٌ كَانَ يَنْزِلُ عَلَيْهِمْ اَلشَّيْطَانُ فِي كُلِّ حَيٍّ وَاحِدٌ

Na Jaabir  (رضي الله عنه)  amesema: Twaaghuwt ni kuhani (mtabiri wa mambo ya ghayb) shaytwaan huwateremkia na kila kabila lina mmoja wao.

 

 وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَال: ((اِجْتَنِبُوا اَلسَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ))  قَالُوا يَا رَسُولَ اَللَّهِ! وَمَا هُنَّ؟ قَالَ: ((اَلشِّرْكُ بِاَللَّهِ، وَالسِّحْرُ، وَقَتْلُ اَلنَّفْسِ اَلَّتِي حَرَّمَ اَللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ، وَأَكْلُ اَلرِّبَا، وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ، وَالتَّوَلِّي يَوْمَ اَلزَّحْفِ، وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْغَافِلاتِ الْمُؤْمِنَاتِ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akawaambia: ((Ni kumshirikisha Allaah, uchawi, kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa kupambana na adui na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَعنْ جُنْدَبٍ مَرْفُوعًا: ((حَدُّ اَلسَّاحِرِ ضَرْبَةٌ بِالسَّيْفِ)) رَوَاهُ التِّزْمِذِيُّ وَقَالَ: اَلصَّحِيحُ أَنَّهُ مَوْقُوفٌ

Na Imepokelewa kutoka kwa Junub (رضي الله عنه)  Hadiyth ifuatayo ikiwa ni Marfuw’: ((Adhabu ya mchawi kupigwa upanga [auliwe])) [At-Tirmidhy na amesema Swahiyh lakini ni Mawquwf]

 

وَفِي صَحِيحِ الْبُخَارِيِّ: عَنْ بَجَالَةَ بْنِ عَبَدَةَ قَالَ: كَتَبَ عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْه) أَنِ اُقْتُلُوا كُلَّ سَاحِرٍ وَسَاحِرَةٍ. قَالَ: فَقَتَلْنَا ثَلاثَ سَوَاحِرَ.

Na katika Swahiyh Al-Bukhaariy kutoka kwa Bajaalah bin ‘Abadah amesema: ‘Umar bin Al-Khattwaab(رضي الله عنه)  aliandika kwamba: “Uweni kila mchawi mwanamme na mchawi mwanamke.” Akasema [Bajaalah]: “Tukaua wachawi watatu.”

 

وَصَحَّ عَنْ حَفْصَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا) أَنَّهَا أَمَرَتْ بِقَتْلِ جَارِيَةٍ لَهَا سَحَرَتْهَا فَقُتِلَتْ. وَكَذَلِكَ صَحَّ عَنْ جُنْدَبٍ

Na Hafswah(رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا)  amesimulia kwamba aliamrisha auliwe mjakazi wake alimroga. Amethibitisha haya Jundab(رضي الله عنه) .

 

قَالَ أَحْمَدُ عَنْ ثَلاثَةٍ مِنْ أَصْحَابِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم  

(Imaam) Ahmad amethibitisha pia kuuliwa kwa wachawi kutoka kwa Maswahaba watatu wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) (‘Umar, Hafswah, Jundub).

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Baqarah (2: 102).

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah An-Nisaa (4: 51).

 

3-Maana ya Al-Jibt na Atw-Twaaghuwt na tofauti baina yake.

 

4-Atw-Twaaghuwt wanaweza kuwa ni miongoni mwa majini au bin Aadam.

 

5-Maelezo ya mambo saba yanayoangamiza yaliyoharamishwa.

 

6-Watabiri na makuhani na wachawi ni makafiri.

 

7-Makuhani na wachawi wauawe na hakuna kuombwa kutubia.

 

8-Ikiwa, makuhani, wachawi walipatikana kwa Waislamu zama za ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه) seuze basi baada ya hapo?   

 

 

Share