Skip navigation.
Home kabah

Duaa Mbali Mbali Za Mtume صلى الله عليه وآله وسلم

 

 

Du'aa ya  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  baada ya kutoka Twaaif

  

اَلَّلهُمَّ إِنِّي  أَشْكُو إِلَيْكَ ضَعْفَ قُُوَّتِي, وَقِلَّةَ حِيْلَتِي, وَهَوَانِي عَلَى النَّاسِ,  يَا أَرْحَمَ الرَّاحِمِين, أَنْتَ رَبُّ الْمُسْتَضْعَفِينَ وَاَنْتَ رَبّي إِلَى مَنْ تَكِلْنِي؟ إِلَى بَعِيدٍ يَتَجَهَّمُنِي أَمٍ إِلَى عَدُوٍ مَلَّكْتَهُ أَمْرِي؟ إِنْ لَمْ يَكُنْ بِكَ غَضَبٌ عَلَىَّ فَلاَ أُبَاِلي، وَلَكِنَّ عَافِيَتَكَ أَوْسَعُ لِي مِنْ ذُنُوبِي,  أَسْأَلُكَ بِنُورِ وَجْهِكَ الَّذِي أَشْرَقَتْ لَهُ الظُّلُمَاتُ، وَصَلَحَ عَلَيْهِ أَمْرُ الدُّنْيَا وَالأَخِرَةِ مِنْ أَنْ يُنْزِلَ عَلَيَّ غَضَبُكَ أَوْ يَحُِلَّ عَلَىَّ سَخَطُُكَ   وَلاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِكَ      

 

 

Allaahumma Inniy Ashkuu Ilayka Dhwa'fa Quwwatiy, Wa Qillata HiylatiyWa Hawaaniy 'Alan-Naas.  Yaa Arhamar-Raahimiyn.  Anta Rabbul-Mustadhw'afiyn, Wa Anta Rabbiy  Ilaa Man Takilniy?  Ilaa Ba'iydin Yatajahhamuniy? Am Ilaa 'Aduwwim-Mallaktahu Amriy?  In-lam Yakun Bika Ghadhwabun 'Alayya Falaa UbaaliyWa Laakin 'Aafiyataka Awsa'u Liy Min Dhunuubiy.  As-aluka Binuuri Wajhika-lladhiy Ashraqat Lahudh-Dhwulumaat, Wa  Swalaha 'Alayhi Amrud-Duniyaa Wal-Aakhiratiy Min Ay-yunzila 'Alayya Ghadhwabuka Aw Yahillu 'Alayya Sakhatwuka, Wa Laa Hawlaa Walaa Quwwata Illaa Bik.  

 

 

Ya Allaah , Kwako peke yako nalalamika udhaifu wa nguvu zangu, na uchache  wa uwezo wangu na unyonge wangu (wa kukabili adha) za watu.  Wewe ndiye mwenye  wingi wa Rehma na wingi wa huruma na upole.

Wewe  ni Mola wa wasiojiweza na wadhaifu.  Nawe ni Mola Wangu.  Unanitupa kwenye mikono ya nani (atakayenisaidia)?  Kwenye mikono ya jamaa  yangu aliye mbali na asiye na huruma na mimi?  Ambaye ananihamakia  kwa chuki na kunidharau?  Au kwenye adui aliyepewa utawala juu ya mambo yangu?  Lakini kama ghadhabu Yako  haitoanguka kwangu au haitonifikia basi hakuna kitu nitakachojali, Na hakika msamaha Wako ni mkubwa kuliko dhambi zangu.     

Nakuomba  kutokana na Nuru ya Wajihi wako, ambayo inaangazia mbingu na inaondoa kiza na kutawala  mambo yote ya dunia na akhera ili hasira Yako isinifikie au ghadhabu Yako isiniangukie.  Na hakuna mamlaka wala nguvu na uwezo ila Wako peke yako.