090-Aayah Na Mafunzo: Sababu Ya Kuteremshwa Aayah Kuhusu Walioritadi Na Kurudia Tena

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Sababu Ya Kuteremshwa Aayah Kuhusu Walioritadi Na Kurudia Tena

 

 

 إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ ثُمَّ ازْدَادُوا كُفْرًا لَّن تُقْبَلَ تَوْبَتُهُمْ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الضَّالُّونَ ﴿٩٠﴾ 

90. Hakika wale waliokufuru baada ya kuamini kwao kisha wakazidi kukufuru; haitokubaliwa tawbah yao, na hao ndio waliopotoka.

 

Mafunzo:

 

Sababun-Nuzuwl: Aayah hii imeteremshwa kuhusu watu waliosilimu kisha wakaritadi kisha wakasilimu tena kisha wakaritadi. Wakatuma watu wao kuuilizia kuhusu jambo hili wakamuuliza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), kisha hapo ikateremka Aayah hii: “Hakika wale waliokufuru baada ya kuamini kwao kisha wakazidi kukufuru; haitokubaliwa tawbah yao, na hao ndio waliopotoka.” (3: 90)  [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) ameipokea Al-Haafidhw Abuu Bakr Al-Bazzaar – Tafsiyr Ibn Kathiyr].

 

 

 

Share