105-Aayah Na Mafunzo: Makundi Sabini Na Tatu Yataingia Motoni Isipokuwa Moja Tu.

 

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

 

Makundi Sabini Na Tatu Yataingia Motoni Isipokuwa Moja Tu

 

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ تَفَرَّقُوا وَاخْتَلَفُوا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ ۚ وَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿١٠٥﴾

Na wala msiwe kama wale waliofarikiana na wakakhitilafiana baada ya kuwajia hoja bayana. Na hao watapata adhabu kuu. [Aal-'Imraan: 105]

 

Mafunzo:

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Wamegawanyika Mayahudi katika mapote sabini na moja na wakagawanyika Manaswara katika mapote sabini na mbili na Ummah wangu utagawanyika mapote sabini na tatu. Yote hayo yataingia motoni ila moja tu.” Maswahaba waliuliza: Ni lipi hilo ee Rasuli wa Allaah?  Akasema: “Ni lile nililokuwemo mimi na Maswahaba zangu.” [Ahmad, Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na Ad-Daarimiy].

 

Share