118-Aayah Na Mafunzo: Kila Nabiy Au Khaliyfah Alikuwa Na Rafiki Mwandani Wawili

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Kila Nabiy Au Khaliyfah Alikuwa Na Rafiki Mwandani Wawili 

Alhidaaya.com

 

 

 Anasema Allaah ('Azza wa Jalla):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا بِطَانَةً مِّن دُونِكُمْ لَا يَأْلُونَكُمْ خَبَالًا وَدُّوا مَا عَنِتُّمْ قَدْ بَدَتِ الْبَغْضَاءُ مِنْ أَفْوَاهِهِمْ وَمَا تُخْفِي صُدُورُهُمْ أَكْبَرُ ۚ قَدْ بَيَّنَّا لَكُمُ الْآيَاتِ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ ﴿١١٨﴾

118. Enyi walioamini! Msifanye rafiki mwandani na msiri (wenu) wasiokuwa nyinyi. Hawatoacha kukuharibieni. Wanatamani kama mngetaabika. Imekwishajitokeza bughudha kutoka midomoni mwao. Na yale yanayoficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Aayaat, (ishara, hoja, dalili) mkiwa mtatia akilini.

 

Mafunzo:

 

Abuu Sa’iyd (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Allaah Hakutuma Nabiy yeyote wala hakumweka Khaliyfah yeyote isipokuwa alikuwa na rafiki mwandani wawili; mmoja anayeamrisha ya kheri na kumsisitiza nayo, na mwengine akiamrisha maovu na kumchochea nayo. Na Al-Ma’swuwm (aliyehifahdiwa asikosee) ni ambaye ma’swuwm (amehifadhiwa asisokee) na Allaah.” [Al-Bukhaariy na An-Nasaaiy].

Share