097-Asbaabun-Nuzuwl: An-Nisaa Aayah 097: إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

An-Nisaa 097-Hakika wale ambao Malaika wanawafisha hali ya kuwa …

 

إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾

Hakika wale ambao Malaika wanawafisha, hali ya kuwa wamejidhulumu nafsi zao, (Malaika) watawaambia: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi.  (Malaika) Watasema: Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia!

 

 

إِلَّا الْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ لَا يَسْتَطِيعُونَ حِيلَةً وَلَا يَهْتَدُونَ سَبِيلًا ﴿٩٨﴾

Isipokuwa wale waliokandamizwa kati ya wanaume na wanawake na watoto ambao hawakuweza kupata hila yoyote wala hawawezi kuongoza njia. (4:97-98)

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremka kama alivyohadithia Muhammad bin ‘Abdir-Rahmaan bin Al-Aswad (رضي الله عنه) kwamba: Watu wa Madiynah walilazimishwa kuandaa jeshi (kupigana na watu wa Ash-Shaam katika khilaafah ya Ibn Az-Zubayr Makkah) na nikawa nimeandikwa humo. Kisha nikakutana na ‘Ikrimah, mtumwa wa Ibn ‘Abbaas aliyekuwa huru, nikamjulisha (hayo), akanikataza mno (kuingia katika orodha ya jeshi), akasema: Ibn ‘Abbaas amenijulisha kwamba baadhi wa Waislamu walikuwa na washirikina hivyo wakikithiri idadi ya washirikina dhidi ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Mshale ulikuwa unarushwa ambao ulimpiga mmoja wao (Waislamu wakiwa pamoja na washirikina) na kumuua, au hupigwa na kuuliwa (kwa upanga).” Hapo Allaah Akateremsha:

 

إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾

Hakika wale ambao Malaika wanawafisha, hali ya kuwa wamejidhulumu nafsi zao, (Malaika) watawaambia: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi.  (Malaika) Watasema: Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia! (4:97)

 

Abuu Aswad akaongezea:

 

إِلَّا الْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ وَالْوِلْدَانِ لَا يَسْتَطِيعُونَ حِيلَةً وَلَا يَهْتَدُونَ سَبِيلًا ﴿٩٨﴾

Isipokuwa wale waliokandamizwa kati ya wanaume na wanawake na watoto ambao hawakuweza kupata hila yoyote wala hawawezi kuongoza njia. (4:98) [Al-Bukhaariy]

 

 

Pia Adhw-Dhwahaak amesema kwamba Aayah hii imeteremshwa kuhusu baadhi ya wanafiki ambao hawakuungana na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), bali walibakia Makkah kisha wakatoka na washirikina katika vita vya Badr. Wakauawa pamoja na waliouawa. Hapo Aayah hii

 

إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾

Hakika wale ambao Malaika wanawafisha, hali ya kuwa wamejidhulumu nafsi zao, (Malaika) watawaambia: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi.  (Malaika) Watasema: Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia! (4:97)

 

Ikateremshwa kuhusu hao waliobakia pamoja na washirikina hali ya kuwa waliweza kufanya hijrah lakini hawakufanya na wakashindwa kuthibitisha Uislamu wao. Watu kama hao wamejidhulumu nafsi zao na wakaingia katika uharamisho kama ilivyokubalika na Ijmaa’ na kutokana na Kauli ya Allaah:

 

إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾

Hakika wale ambao Malaika wanawafisha, hali ya kuwa wamejidhulumu nafsi zao, (Malaika) watawaambia: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi.  (Malaika) Watasema: Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia! (4:97)

 

 

 

 

 

Share