181-Aayah Na Mafunzo: Kundi Katika Ummah Huu Watabakia Katika Haki Mpaka Siku Ya Qiyaamah

 

Aayah Na Mafunzo

 

www.alhidaaya.com

 

Al-A’raaf 181

 

181-Kundi Katika Ummah Huu Watabakia Katika Haki Mpaka Siku Ya Qiyaamah

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمِمَّنْ خَلَقْنَا أُمَّةٌ يَهْدُونَ بِالْحَقِّ وَبِهِ يَعْدِلُونَ ﴿١٨١﴾

Na katika Tuliowaumba, wako ummah wanaoongoza kwa haki na kwayo wanahukumu kiadilifu. [Al-A'raaf: 181]

 

 

Mafunzo:

Amesimulia Mu’aawiyah bin Abiy Sufyaan (رضي الله عنه) : Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Kutakuweko kundi katika Ummah wangu litaendelea kuwa juu ya haki likiwa na nguvu, hawezi kuwadhuru yeyote aliyekwenda nao kinyume au aliyesaliti mpaka Siku ya Qiyaamah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share