09-Shaykh Swaalih Al-Fawzaan: Kusoma Du’aa Zisizothibiti Na Kwa Mkusanyiko Wa Watu Katika Twawaaf

 

Kusoma Du’aa Zisizothibiti Na Kwa Mkusanyiko Wa Watu Katika Twawaaf

 

 Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Makosa gani yanayotendekea katika twawaaf?

 

JIBU:

 

Hujaji wanasoma du'aa mahsusi wanapofanya twawaaf. Na wengi wao wanakuwa katika vikundi, kisha mmoja wao anayewaongoza husoma hizo du'aa na wengine wanakariri kwa mkarara mmoja. Haya ni makosa katika vipengele viwili;

 

Kwanza:

 

Hivyo ni kufuata du'aa ambazo hazimo katika mafunzo ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika twawaaf.

 

Pili:

 

Kuomba du'aa katika kikundi kwa mkarara ni bid’ah (uzushi). Juu ya hivyo ni kusababisha tashwishi kwa Hujaji wengine wanaofanya twawaaf. Shariy’ah inampasa kila mmoja asome du'aa yake bila ya kupandisha sauti.

 

 

[Al-Bid’ah wal-Muhdathaat wa maa laa aswla lahu – Uk. 398. Al-Fataawa Fadhwiylatush-Shaykh Swaalih Ibn Fawzaan al-Fawzaan – Mjalada 2, Uk. 30]

 

 

 

 

Share