04-Imaam Ibn Baaz: Kupaka Manukato Katika Ihraam

 

 

 Kupaka Manukato Katika Ihraam

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nini hukmu ya kupata mafuta mazuri katika ihraam kabla ya kutia nia na talbiyah?

 

JIBU:

 

Sio sawa kupaka manukato mazuri katika ihraam (vipande viwili vyeupe vya shuka vinavyovaliwa). Sunnah ni kupaka mafuta mazuri mwilini kama kichwani, ndevu, kwapani na sehemu nyingine. Ama ihraam haipakwi mafuta mazuri kutokana na kauli ya Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Msivae nguo zilizoguswa na az-za’faraan au al-wars [aina ya mafuta mazuri]))

 

Kwa hiyo Sunnah ni kujipaka mafuta mazuri mwilini pekee na sio katika ihraam. Na ikiwa imepakwa, basi isivaliwe bali ioshwe au mtu abadlishe avae nyingineyo.

 

[Majmuw' Fataawaa Samaahat  Shaykh Ibn Baaz – Mjalada 6, Uk 96, Fatwa 46]

 

 

Tanbihi Kutoka Alhidaaya:

 

Hukmu hiyo ya kupaka mafuta mazuri inawahusu wanaume pekee kwani mwanamke haimpasi kujipaka mafuta mazuri kabisa akiwa Hajj au hata anapokuwa nje ya Hajj kwani jambo hilo limekatazwa kuwa mwanamke asitoke nje akiwa amejipaka mafuta mazuri ili isiwe fitna kwa wanaume watakaosikia harufu nzuri kwake.

 

 

Share