02-Shaykh Swaalih Al-Fawzaan: Kumfanyia Hajj Mtu Kwa Ajili Ya Kupokea Ujira

 

 

Kumfanyia Hajj Mtu Kwa Ajili Ya Kupokea Ujira

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Je, inaruhusiwa kumfanyia mtu nguzo ya Hajj ambaye anao uwezo wa kifedha na siha kutekeleza mwenyewe Hajj, kwa ajili ya kupata ujira kwake?

 

JIBU:

 

 

Yeyote mwenye uwezo wa kutekeleza mwenyewe nguzo ya Hajj, basi haimpasi kumuwakilisha mtu mwingine kumfanyia Hajj, na hatopata thawabu kutoka kwa Allaah kufanya hivyo.

 

Ama ikiwa mtu hana uwezo wa kufanya mwenyewe Hajj kutokana na hali ya kudumu inayomzuia kutekeleza fardhi hiyo, basi inaruhusiwa kumuwakilisha mtu mwingine kumfanyia Hajj.

 

Na hakuna ubaya kupokea ujira (kwa ajili ya kumfanyia mtu Hajj) ikiwa atautumia ujira huo kwa ajili ya Hajj na sio kwa ajili ya kutafuta uchumi wa fedha na kuzitumia katika mambo ya starehe. Tunayo hukmu ambayo baadhi ya ‘Ulamaa wametumia ambayo imetokana na dalili sahihi kwamba: “Yeyote mwenye kutia niyyah ya kufanya Hajj kwa ajili ya uchumi, basi asifanye. Na mwenye kupokea ujira kwa ajili ya kumfanyia mtu Hajj basi anaweza kufanya hivyo.” 

 

[Majmuw' al-Fataawa Ibn Taymiyyah, Mjadala 26, Uk. 19]

 

Na maana ya hii ni kwamba, yeyote atakayetumia pesa kwa ajili ya kufanya Hajj (matumizi ya Hajj) basi hakuna ubaya lakini yeyote mwenye kufanya Hajj kwa ajili ya kuchuma fedha basi hairuhusiwi.  

 

 

[Shaykh Swaalih ibn Fawazaan - Al-Muntaqaa min Fataawa Shaykh Swaalih al-Fawzaan – Mjalada 3, Uk. 190, Fatwa Namba 291].

 

Share