04-Shaykh Swaalih Al-Fawzaan : Kumfanyia ‘Umrah Kaka Aliyefariki

 

Kumfanyia ‘Umrah Kaka Aliyefariki

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nimetia nia kumfanyia 'Umrah kaka yangu mkubwa tokea alipofariki. Hivi sasa umefika wakati wa kuweza kumfanyia. Je, kitendo hiki kinafaa katika mafunzo ya dini kuwa thawabu zitamfikia yeye aliyefariki?

 

JIBU:

 

 

Ndio, kwa sababu kitendo chema cha kumfanyia 'Umrah kaka yako aliyefariki ikiwa ni 'Umrah ya fardh (inayoambatana na Hajj) au 'Umrah ya Sunnah (inayopendekezeka). Kwa hiyo hiki ni kitendo kikubwa kizuri. Lakini (kutekeleza huko hiyo 'Umrah) iwe kwa sharti kuwa kwanza wewe mwenyewe umeshatekeleza 'Umrah ya fardhi.

 

Na Allah Anajua zaidi

 

 

[Al-Muntaqaa min Fataawa Shaykh Swaalih Al-Fawzaan – Mjalada 5, Uk. 160, Fatwa Namba 240].

 

Share