05-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Kumpa Mtu Zawadi Kwa Ajili Ya Kumfanyia Twawaaf

 

Kumpa Mtu Zawadi Kwa Ajili Ya Kumfanyia Twawaaf

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nini hukmu ya kumpa mtu zawadi kwa ajili ya kumfanyia mtu mwengine twawaaf. Humwendea mtu na kumwambia "Nifanyie saba" (yaani twawaaf saba) akitegemea thawabu zimfikie yeye mwenyewe. Je, inaruhusiwa?

 

 

JIBU:

 

 

Hairuhusiwi kufanya twawaaf katika Ka’bah kwa ajili ya mtu mwengine. Kwa hiyo mtu yeyote asifanye hivyo ila akiwa anamfanyia mtu fardhi ya Hajj au 'Umrah. Hivyo ni kutekeleza taratibu zote kwa niyyah ya huyo mtu.

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 [Fataawa al-Lajnah ad-Daaimah lil-Buhuwth al-'Ilmiyyah wal-Iftaa. Mjalada 11, Uk. 236, Fatwa Namba 8433 -   Imejumuisha:

 

Kiongozi Mkuu: Shaykh ‘Abdul-’Aziyz bin ‘Abdillaah bin Baaz

 

Msaidizi Kiongozi Mkuu: Shaykh ‘Abdur-Razzaaq 'Afiyfiy

 

Mjumbe: Shaykh ‘Abdullaah bin Ghudayyaan

 

Mjumbe: Shaykh ‘Abdullaah bin Qu’uwd]

 

 

Share