Skip navigation.
Home kabah

Siku Macho Nikifumba (Sisitizo)

Twaha H. M Kiobya [Mujaahid]

TIOT Morogoro

 1.  Bismillah naanza, kwa jina la utukufu

        Nia watu kuwafunza, Natumia hii safu

         Niepushe ya kuponza, wafanye uadilifu

               Hayatasaidia wafu, Masadaka ya matanga

 

 

          2. Uloyatenda mwenyewe, kabla ya kutawafu

Mazuri au yasiwe, atakulipa Raufu

           Hata kama usomewe, mahitaji maradufu

Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga

 

3. Wale nyama au sunga, hayafuti ulanifu

                   Hawawezi pata mwanga, wale washibe wakinifu

        Haya ninyi mwajivunga, tatu hazifiki wafu

           Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga

 

4. Ni uzushi kwenye dini, hajasema Ashrafu

           Si kitu arobaini, utapooza minofu

          Wale wakudanganyeni, ma vyakula na sarafu

       Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga

 

 

5. Msimbe hayo yashike, mshairi maarufu

    Kwenye uzushi utoke, ufate wasadikifu

  Usingoje uumbuke, ya uzushi ni uchafu

          Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga