Mashairi - Nguzo Za Kiislamu, Ihsaan Na Imaan
Mtungaji: 'Aliy 'Umar 'Uthmaan
NGUZO ZA UISLAMU,
Nguzo za u-islamu, idadi yake ni tano
Shahadayo muhimu, ulimi na moyo mfano
Upwekesho Karimu, na Muhammad bora mno
Nguzo ya pili ni swala, idumishe maishani
Na ukilekee kibula, kusimamisha dini
Ndilo kwanza suala, taulizwa kaburini
Tatu nayo ni saumu, faradhi Ramadhani
Baleghe memlazimu, popote ulimwenguni
Wenye akili timamu, ielezavyo Qurani
Nguzo ya nne ni zaka, kwa wale wenye
Lazima sidhihaka, si khiari tukubali
Wale waloneemeka, kutofanya ubakhili
Tano kuhiji Makka, kwa yule mwenye uwezo
Mara moja kumbuka, ni ya mtume mafunzo
Mefaulu bila shaka, atimizae hii nguzo
NGUZO YA IHSANI
Nguzo nayo ya ihsani, ni moja tu uielewe
Umuabudu Manani, kwamba umuonawe
Kama wewe humuoni, akuonawe utambue
NGUZO ZA IMANI
Nguzo sita za imani, uzipige makamama
Mola wetu muamini, imara nawe simama
Alotukuka yakini, alotangu ya daima
Amini kuna malaika, japo nawe huwaoni
Uwe na nzito hakika, iyakinishe moyoni
Uondoe zote shaka, msingi wa yetu dini
Kuna vitabu vinne, lazima uvikubali
Tafuta kweli uone, usiwe nawe jahili
Quran ndicho cha nne, Zabur,Taurat,Injili
Usiwabugue mitume, meteremsha Qadimu
Nyuma yao tusimame, kutoka baba Adamu
Muhammadi tumsome, na babuye Ibrahimu
Tuamini na qadari, mipango yake Mola
Asokuwa na mshauri, kumuuliza masuala
Mwenye vazi kiburi, arshini metawala
Kheri zote na shari, zatoka kwake Rabana
Hatuna sisi khiari, lolote yeye kinena
Shukuru na usubiri, upate mama kuvuna
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
