Mukhtasari Wa 'Aqiydah Swahiyh Ya Muislamu - 1
|
SUALI |
JAWABU |
DALILI KUTOKA QUR'AAN |
DALILI KUTOKA HADITHI |
|
1- Kwa nini Allah Katuumba? |
Katuumba Ili tumuabudu na tusimshirikishe Naye kwa chochote. |
(وماخلقت الجن والإنس إلا ليعبدون) Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi (Adhaariyaat 56) |
) حق الله على العباد أن يعبدوه ولا يشركوا به شيئا ( Haki ya Allah kutoka kwa mja wake (mja anapaswa kumfanyia) ni kumuabudu bila ya kumshirikisha |
|
2- Jinsi gani tumuabudu Allaah سبحانه وتعالى |
Kama Alivyotuamrisha Allah na Mtume صلى الله عليه وسلم kwa ikhlaas |
(وما امروا إلا ليعبدوا الله مخلصين له الدين) Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, (Al-Bayyinah 5) |
(من عمل عملا ليس عليه أمرنا فهو رد ) Atakayefanya kitendo kisichokuwa chetu (kisicho katika Dini) kitarudishwa (hakitakubaliwa) |
|
3- Je, tumuabudu Allaah سبحانه وتعالى kwa kumuogopa (adhabu Yake) na kutumaini (pepo Yake)? |
Ndio tunamuabudu kwa kumukhofu na kuwa na matumaini |
(وأدعوه خوفا وطمعا (أي خوفا من ناره وطمعا في جنته Na muombeni kwa kuogopa na kwa kutumai. (kukhofu moto Wake na kutumaini pepo Yake) (A'araf 56 ) |
( اسأل الله الجنة وأعوذ به من النار ) Namuomba Allah Pepo na najikinga Kwake na moto |
|
4- Nini Ihsaan katika ibada? |
Kujichunga (kuwa makini) katika ibada kwa ajili yake Allaah سبحانه وتعالى Pekee. |
(ان الله كان عليكم رقيبا) النساء (الذي يراك حين تقوم) الشعراء Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaangalieni. (An-Nisaa 1) Ambaye anakuona unapo simama,(Ash-Shu'araa 218) |
(الإحسان أن تعبد الله كانك تراه فأن لم تكن تراه فأنه يراك ) Ihsaan ni kumuabudu Allaah سبحانه وتعالى kama vile unamuona, na |
|
5- Kwa nini Allaah سبحانه وتعالى Ametuma Wajumbe (Mitume)? |
Kutuita katika kumuabudu na kuepukana na kumshirikisha |
(ولقد بعثنا في كل أمة رسولا أن اعبدوا الله وأجتنبوا الطاغوت) Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani.(An-Nahl 36) |
) والانبياء إخوة ودينهم واحد( Na Manabii ni ndugu na dini |
|
6- Nini Tawhiid ya Ilaah? |
Kumfanyia Yeye Pekee ibada, dua, nadhiri na Hukumu. |
(فأعلم أنه لا إلاه إلا الله) Basi jua ya kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, (Muhammad 19) |
(فليكن أول ما تدعوهم اليه شهادة أن لا إله إلا الله) Jambo la kwanza liwe mnapowalingania wao Kwake ni "Kuthibitisha kwamba hakuna mola apasaye kuabudiwa isipokuwa Allaah سبحانه وتعالى) |
|
7- Nini maana ya Laa Ilaaha illa Allaah? |
Hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah سبحانه وتعالى. |
(ذلك بأن الله هو الحق وأن مايدعون من دونه الباطل ) Hivi ni kwa sababu hakika Mwenyezi Mungu ndiye wa kweli, na hakika wanacho kiomba ni cha uwongo (Luqman 30) |
(من قال لا إله إلا الله وكفر بما يعبد من دون الله حرم ماله ودمه ) Atakayesema 'Laa ilaaha illa Allah na akawapinga wanaoabudiwa wasio Allaah سبحانه وتعالى italindwa (itakuwa haramu mtu kuchukua) |
|
8- Nini maana ya Tawhiid katika sifa za Allaah سبحانه وتعالى |
Kuthibitisha alivyojisifu Mwenyewe Allaah سبحانه وتعالى au alivyosifiwa na Mtume wake. |
) ليس كمثله شيء وهو السميع البصير) Hapana kitu |
(ينزل ربنا تبارك وتعالى في كل ليلة إلى السماء الدنيا) Mola wetu huteremka kila usiku katika mbingu ya dunia |
|
9- Nini faida ya Tawhiid kwa Muislamu? |
Kupata Hidaaya duniani na kuwa katika amani akhera |
(الذين أمنوا ولم يلبسوا إيمانهم بظلم أولئك لهم الأمن وهم مهتدون ) Wale ambao wameamini, na hawakuchanganya imani |
( حق العباد على الله أن لايعذب من لا يشرك به شيئ ) Haki ya mja kutoka kwa Allaah سبحانه وتعالى (Mwenyeezi Mungu anayomfanyia) kuwa Hamuadhibu yule asiyemshirikisha Yeye na chochote. |
|
10- Je, Allaah سبحانه وتعالى yuko wapi? |
Allaah سبحانه وتعالى yuko mbinguni juu ya 'Arshi |
(الرحمن على العرش أستوى) Ar-Rahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi (Twaha 5) |
) إن الله كتب كتاباً إن رحمتي سبقت غضبي فهو مكتوب عنه فوق العرش ) Allaah سبحانه وتعالى Ameandika maandishi kwamba Rahma yangu imeshinda ghadhabu yangu, nayo yameandikwa kumhusu Yeye juu ya 'Arshi |
|
11- Je, Allaah سبحانه وتعالى yuko na sisi kwa dhati yake au kwa elimu yake? |
Allaah سبحانه وتعالى yuko na sisi kwa elimu yake anatuona na anatusikia |
( قال لا تخافا إنني معكما أسمع وأرى) Akasema: Msiogope! Hakika Mimi ni pamoja nanyi. Nasikia na ninaona (Twaha 46). |
(إنكم تدعون سميعا قريبا وهو معكم) Hakika nyinyi mnamuomba Mwenye kusikia, Aliye karibu na Yeye yuko pamoja nanyi. |
|
12- Dhambi gani ni kubwa kabisa? |
Dhambi kubwa kabisa ni kumshirikisha Allaah سبحانه وتعالى |
(يابني لاتشرك بالله إن الشرك لظلم عظيم) Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu. Kwani hakika ushirikina bila ya shaka ni dhulma iliyo kubwa. (Luqman 13) |
(سئل أي الذنب أعظم؟قال أن تدعو لله ندا وهو خلقك ) Aliulizwa dhambi gani kubwa? Akasema ni kumuomba Allaah pamoja na mshirika Na hali Yeye ndiye Aliyekuumba. |
|
13- Shirki gani iliyokuwa kubwa? |
Kufanya ibada kwa kumuelekea asiye Allaah سبحانه وتعالى |
)قل إنما أدعو ربي ولا أشرك به أحدا( Sema: Hakika mimi namwomba Mola wangu Mlezi, wala simshirikishi Yeye na yeyote (Al-Jinn 20) |
(أكبر الكبائر الإشراك بالله) Dhambi kubwa ni kumshirikisha Allaah سبحانه وتعالى |
|
14- Ni yapi madhara ya kumshirikisha Allaah سبحانه وتعالى |
Kumshirikisha Allaah سبحانه وتعالى husababisha kudumu milele motoni |
(إنه من يشرك بالله فقد حرم الله عليه الجنة وماواه النار) Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni (AL-Maida 72) |
(من مات يشرك بالله شيئا دخل النار) Atakayekufa na huku amemshirikisha Allaah سبحانه وتعالى kwa chochote, ataingia motoni. |
|
15- Je, Kitendo chema kinafaa kikiwa kimemshirikisha Allaah سبحانه وتعالى |
Hakifai kitu kitendo ambacho kina kumshirikisha Allaah سبحانه وتعالى |
(ولو أشركوا لحبط عنهم ما كانوا يعلمون) Na lau wangeli mshirikisha yangeli waharibikia waliyo kuwa wakiyatenda (An-'Aam 88) |
(من عمل عملا أشرك فيه معي غيري تركته وشركه) Atakayefanya kitendo na huku kanishirikisha Mimi kwa kitendo hicho na mwengine, namwacha yeye na shirki yake. |
|
16- Je, Shirki ipo kwa Waislamu? |
Ndio, ni masikitiko kuwa ipo tena nyingi |
(وما يؤمن أكثرهم بالله إلا وهم مشركون) Na wengi katika wao hawamuamini Mwenyezi Mungu pasina kuwa ni washirikina (Yusuf 106) |
(لاتقوم الساعة حتى تلحق قبائل من أمتي بالمشركين وحتى تعبد الأوثان ) Qiyama hakitasimama mpaka kutafika wakati watu wa baadhi ya makabila katika umma wangu wataungana na washirikina na hadi watakapoabudu asiye Allah! |
|
17- Nini hukumu ya kumuomba asiye Allaah سبحانه وتعالى |
Kuwaomba ‘Mawalii’ ni shirki yenye kumpeleka mtu motoni. |
(فلا تدع مع الله الها آخر فتكون من المعذبين) Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa (As-Shu'araa 213) |
(من مات وهو يدعو من دون الله ندا دخل النار) Atakayekufa katika hali kumuomba asiye Allaah سبحانه وتعالى ataingia motoni. |
|
18- Je, Kuomba dua ni ibada ya Allaah سبحانه وتعالى |
Ndio, kuomba duaa ni ibada ya Allaah سبحانه وتعالى |
(وقال ربكم أدعوني استجب لكم) Na Mola wenu Mlezi anasema: Niombeni nitakuitikien (Ghaafir 60) |
(الدعاء هو العبادة ) Dua ni ibada |
|
19- Je, waliokufa wanasikia dua? |
Waliokufa hawasikii dua |
(إنك لا تسمع الموتى ) (وما انت بمسمع من في القبور( Kwa hakika wewe huwezi kuwafanya maiti wasikie,(An-Naml 80) Wala wewe si wa kuwasikilizisha walio makaburini. (Fatir 22) |
(إن لله ملائكة سياحين في الأرض يبلغوني عن أمتي السلام) Hakika Allaah سبحانه وتعالى Anao malaika wanaozunguka katika ardhi wakinifikishia salamu kotoka kwa umma wangu. |
|
20- Je, nafaa tuwaombe maiti na wasiopo watuokoe? |
Hatuwaombi wao watuokoe bali tunamuomba Allaah سبحانه وتعالى |
( اذ تستغيثون ربكم فاستجاب لكم) Mlipo kuwa mkimuomba msaada Mola wenu Mlezi, naye akakujibuni (Al-A'araaf 9) |
(كان إذا أصابه هم أو غم قال: ياحي ياقيوم برحمتك أستغيث) Alikuwa akifikwa na hamu au majonzi anasema 'Ewe uliye na uhai wa maisha, uliyesimamia kila jambo, kwa rahma zako nakuomba uniokoe. |
|
21- Je, Inafaa kuomba msaada pasipo na Allaah? |
Haifai kuomba msaada kwa mwengine asiye Allaah سبحانه وتعالى |
(إياك نعبد وإياك نستعين) Wewe tu ndiye tunayekuabudu na Wewe tu ndiye tunayekuomba msaada (Al-Fatiha 5) |
(إذا سألت فأسال الله وإذا أستعنت فأستعن بالله ) Unapoomba muombe Allaah na unapotaka msaada taka msaada kwa Allaah سبحانه وتعالى |
|
22- Je, Inafaa kuomba msaada kwa walio hai? |
Ndio kwa kadiri wanavyoweza |
(وتعاونوا عل البر والتقوى ولا تعاونوا على الإثم والعدوان) Na msaidiane katika wema na ucha Mungu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui (Al-Maida 2) |
(والله في عون العبد ما دام العبد في عون أخيه ) Allaah سبحانه وتعالى yuko katika kumsaidia mja wake vile anavyoendelea kumsaidia mwenzake. |
|
23- Je, Inafaa kuweka nadhiri pasipo na Allaah سبحانه وتعالى? |
Haipasi kuweka nadhiri isipokuwa kwa sababu ya Allaah سبحانه وتعالى. |
(رب إني نذرت لك ما في بطني محررا فتقبل مني ) Mola wangu Mlezi! Nimekuwekea nadhiri kilichomo tumboni mwangu kuwa wakfu; basi nikubalie. (Al-Imraan 35) |
(من نذر أن يطيع الله فليطعه ومن نذر أين يعصيه فلا يعصه ) Anayeweka nadhiri kumtii Allaah سبحانه وتعالى basi amtii, na aliyeweka nadhiri kumuasi Allaah سبحانه وتعالى basi asimuasi. |
|
24- Je, Inafaa kuchinja bila kumkusudia Allaah سبحانه وتعالى? |
Haifai kuchinja kwa malengo yasiyo ya Allaah سبحانه وتعالى kwa sababu ni shirki kubwa. |
(فصل لربك وأنحر) Basi sali na uchinje kwa ajili ya Mola wako Mlezi (Al-Kauthar 2) |
(لعن الله من ذبح لغير الله( Allaah سبحانه وتعالى humlaani anayechinja bila ya sababu ya Allaah سبحانه وتعالى. |
|
25- Je, Inafaa kutufu makaburi? |
Haifai kuzunguka makaburi, bali kuzunguka (kutufu) Kaaba pekee. |
(وليطوفوا بالبيت العتيق ) na waizunguke Nyumba ya Kale (Al-Hajj 29) |
(من طاف بالبيت سبعا وصلى ركعتين كان كعتق رقبة ) Atakayezunguka Kaaba mara saba kisha akaswali rakaa mbili ni |
|
26- Je, Inafaa kuswali na kaburi liko mbele yako? |
Haifai kuswali kulielekea kaburi. |
(فول وجهك شطر المسجد الحرام ( Basi elekeza uso wako upande wa Msikiti Mtakatifu (Al-Baqara 144) |
(لاتجلسوا على القبور ولا تصلوا إليها) Msikalie makaburi wala msiswali kuyaelekea. |
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
