SWALI:
asalam aleikum.
swali langu ni najiona siku zinavyo zidi kenda najiona imani yangu inapungua nakuwa mzito wakufanya ibada na kusoma quraan, nina ogopa nisije nikaendelea hivihivi. naombeni mnisaidie nifanye nini? niweze kurudi katika msimamo mzuri wa dini.
na alaah awajaalia kila la kheri kwa kazi mnayo fanya ya kuelimisha watu
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Tunapenda kujulisha kwamba mja anapotambua kuwa imani yake inakuwa dhaifu na anapotaka kujua njia za kujikurubisha na Mola wake ni dalili ya uongofu na kupendwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala). Kwani wangapi wanakuwa katika hali kama hiyo lakini hawatambui wala kujali bali kuacha nafsi zao ziendelee kuridhisha matamanio yake.
Hivyo inakupasa kwanza kumshukuru Mola wako Mtukufu kwa kukutanabahisha kabla ya kutumbukia kabisa katika upotofu.
Pili fanya yafuatayo ili usalimike na urudishe hali yako katika usalama na taqwa:
Hiswnul-Muslim: Du’aa Na Adhkaar Kusoma Na Kwa Kusikiliza (Toleo Lilohaririwa) [2]
027-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni [3]
Tunatumai kwamba utayatekeleza hayo tuliyokuarifu, na tunaomba kuwa yakufae, na Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Azidi Kukuongoza Akutoe katika kiza unachokaribia kuingia na Akuweke katika nuru na Akujaalie uwe katika waja Wake Wema.
Na Allaah Anajua zaidi
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/67
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/node/7128
[3] http://www.alhidaaya.com/sw/node/9758
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F2589&title=Imani%20Yangu%20Inapungua%20Nakhofu%20Kupotoka%20Nifanyeje%3F