SWALI:
ASALAMU ALAYKUM.
Swali Langu hili, kwa kawaida huwa ninaposoma, mambo ya dini kwa mfano makala ua ninapo sikiliza mawaidha au kusoma Qur-ani hutokezea ndani ya nafsi yangu kusema jambo hili ni uongo yaani huwa sitamki mdomoni mwangu moyo tu hunipiga paa nakusema iwe Mtume Swala lwahu Alayhi Wasalamu amesema hivi haiwezekani. Halafu hushtuka na kusema ASTAHAFIRULLAH. Naomba jawabu ndugu zanguni Waislamu. NIFANYE NINI MIE JAMANI? Kwa sababu hujihisi ibada zangu zote zinaharibika.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kutiwa katika wasiwasi. Hakika wasiwasi huu unaingizwa bila ya kuwa na haja katika hilo. Hata hivyo, wanadamu huwa wanaingia katika mtego huo kwa sababu moja au nyingine. Wasiwasi huu huingia kwa mwanaadamu, hasa akiwa:
Kitu ambacho unatakiwa kufanya ni kama ifuatavyo:
027-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni [2]
Na du’aa zote nyinginezo unazohitaji katika hali yako utazipata katika kitabu kifuatacho:
Hiswnul-Muslim: Du’aa Na Adhkaar Kusoma Na Kwa Kusikiliza (Toleo Lilohaririwa) [3]
Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Akuondoshe katika wasiwasi ulionao na akuweke katika hali ya Imani ya daima na Akuongoze wewe na sisi katika njia Yake nyoofu.
Na Allaah Anajua zaidi
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/67
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/node/9758
[3] http://www.alhidaaya.com/sw/node/7128
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F3301&title=Wasiwasi%20Wa%20Shaytwaan%20Unamfanya%20Afikirie%20Mambo%20Ya%20Kufru%2C%20Afanyeje%3F