Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
49-Nabiy Pekee Aliyepewa Kauli Za Kusherehi Kitabu Chake
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الذِّكْرَ لِتُبَيِّنَ لِلنَّاسِ مَا نُزِّلَ إِلَيْهِمْ وَلَعَلَّهُمْ يَتَفَكَّرُونَ﴿٤٤﴾
(Tumewatuma) Kwa hoja bayana na vitabu. Na Tumekuteremshia Ukumbusho (Qur-aan) ili uwabainishie watu yaliyoteremshwa kwao huenda wakapata kutafakari. [An-Nahl: 44]
Maana yake: “Tumekuteremshia Qur-aan ee Rasuli, ili uwabainishie wazi watu yaliyofichikia katika maana zake, hukmu zake na ili wazingatie (Aayaat) na waongoke kwayo.” [Tafsiyr Al-Muyassar]
Hivyo basi anayoyasema katika kusherehi Aayaat za Qur-aan ni Wahyi Aliofunuliwa Na Allaah (سبحانه وتعالى) Ambaye Anasema:
مَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ﴿٣﴾
Na wala hatamki kwa hawaa.
إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ ﴿٤﴾
Hayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa. [An-Najm: 3-4]
Akasema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuthibitisha hayo katika Hadiyth:
((أَلَا إِنِّي أُوتِيتُ الْقُرْآنَ وَمِثْلَهُ مَعَهُ)) صحيح رواه أبو داود
((Hakika mimi nimepewa Qur-aan na mfano wake)) [Hadiyth Swahiyh, Abuu Daawuwd]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10297&title=49-Fadhila%20Za%20Nabiy%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%3A%20Nabiy%20Pekee%20Aliyepewa%20Kauli%20Za%20Kusherehi%20Kitabu%20Chake%20