Sababu Za Kuteremshwa
(Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
016-Suwrah An-Nahl
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [2]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
016-Suwrah An-Nahl Aayah 75 - 76
Kauli Zake Allaah (سبحانه وتعالى):
ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا عَبْدًا مَّمْلُوكًا لَّا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَمَن رَّزَقْنَاهُ مِنَّا رِزْقًا حَسَنًا فَهُوَ يُنفِقُ مِنْهُ سِرًّا وَجَهْرًا ۖ هَلْ يَسْتَوُونَ ۚ الْحَمْدُ لِلَّـهِ ۚ بَلْ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ﴿٧٥﴾
Allaah Amepiga mfano wa mja anayemilikiwa hana uwezo juu ya chochote na (mwengine) ambaye Tumemruzuku kutoka Kwetu riziki nzuri; naye anatoa katika humo kwa siri na dhahiri. Je, wanalingana sawa? AlhamduliLLaah (Himidi Anastahiki Allaah!). Bali wengi wao hawajui.
وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا رَّجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا أَبْكَمُ لَا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَهُوَ كَلٌّ عَلَىٰ مَوْلَاهُ أَيْنَمَا يُوَجِّههُّ لَا يَأْتِ بِخَيْرٍ ۖ هَلْ يَسْتَوِي هُوَ وَمَن يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ ۙ وَهُوَ عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿٧٦﴾
Na Allaah amepiga mfano (mwingine) wa watu wawili; mmoja ni bubu asiye na uwezo juu ya chochote naye ni mzigo kwa bwana wake, popote unapomuelekeza haleti khayr. Je, analingana sawa yeye na yule anayeamrisha uadilifu, naye yuko juu ya njia iliyonyooka? [An-Nahl: 75-76]
Sababun-Nuzuwl:
عن ابن عباس في قوله عز وجل ((ضَرَبَ اللَّهُ مَثَلاً عَبْداً مَمْلُوكاً ..)) قال: نزلت في رجل من قريش وعبده، وفي قوله ((مَثَلًا رَجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا أَبْكَمُ لا يَقْدِرُ عَلَى شَيْءٍ)) إلى قوله ((وَهُوَ عَلَى صِرَاطٍ مُسْتَقِيمٍ)). قال هو عثمان بن عفان، قال: والأبكم الذي أينما يوجهه لا يأتي بخير، ذاك مولى عثمان بن عفان كان عثمان ينفق عليه ويكفله ويكفيه المؤونة، وكان الآخر يكره الإسلام ويأباه، وينهاه عن الصدقة والمعروف فنزلت فيهما.
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas kuhusu Kauli ya Allaah:
ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا عَبْدًا مَّمْلُوكًا
Allaah Amepiga mfano wa mja anayemilikiwa…
Amesema imeteremka kuhusu mtu katika Quraysh na mtumwa wake.
Na kuhusu Kauli Yake:
مَثَلًا رَّجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا أَبْكَمُ لَا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ
Mfano (mwingine) wa watu wawili; mmoja ni bubu asiye na uwezo juu ya chochote…
mpaka kauli Yake:
وَهُوَ عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ
naye yuko juu ya njia iliyonyooka.
Amesema: “(Aaliyekusudiwa) huyo ni ‘Uthmaan bin ‘Affaan.”
Akasema pia: “Na bubu ambaye popote unapomuelekeza haleti khayr, huyo ni mtumwa wa ‘Uthmaan, alikuwa ‘Uthmaan akimhudumia matumizi yake na kumdhamini, na kumtosheleza chakula chake. Na yule (mtumwa) mwengine (wa Aayah iliyotangulia) alichukia Uislamu na akaukanusha na akimzuia (bwana wake) asitoe Swadaqah na kutokufanya wema, zikateremka (Hizo Aayah) kuhusu wao wawili:
[Imaam Al-Muqbil amerekodi Ibn Jariyr (4/151) na watu wake ni watu Swahiyh]
Na pia,
عن إبراهيم، عن عكرمة، عن ابن عباس قال: نزلت هذه الآية ((ضَرَبَ اللَّهُ مَثَلاً عَبْداً مَمْلُوكاً لا يَقْدِرُ عَلَى شَيْءٍ )) في هِشَامِ بْنِ عَمْرٍو، وَهُوَ الَّذِي يُنْفِقُ مَالَهُ سِرًّا وَجَهْرًا، وَمَوْلَاهُ أَبُو الْجَوْزَاءِ الَّذِي كَانَ يَنْهَاهُ وَنَزَلَتْ (( وَضَرَبَ اللَّهُ مَثَلاً رَجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا أَبْكَمُ لا يَقْدِرُ عَلَى شَيْءٍ )) فَالْأَبْكَمُ مِنْهُمَا الْكَلُّ عَلَى مَوْلَاهُ هُوَ أُسَيْدُ بْنُ أَبِي الْعِيصِ، وَالَّذِي يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَهُوَ عَلَى صِرَاطٍ مُسْتَقِيمٍ هُوَ عُثْمَانُ بْنُ عَفَّانَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ
Kutoka kwa Ibraahiym kutoka kwa Ikrimah kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: Zimeteremka Aayah hizi mbili:
ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا عَبْدًا مَّمْلُوكًا لَّا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ
Allaah Amepiga mfano wa mja anayemilikiwa hana uwezo juu ya chochote…
Kumhusu Hishaam ambaye alikuwa akitoa mali yake kwa siri na kwa dhahiri na mtumwa wake Abu Al-Jawzaaiy alimzuia asifanye hivyo, basi ikateremka:
وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا رَّجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا أَبْكَمُ لَا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَهُوَ كَلٌّ عَلَىٰ مَوْلَاهُ أَيْنَمَا يُوَجِّههُّ لَا يَأْتِ بِخَيْرٍ ۖ هَلْ يَسْتَوِي هُوَ وَمَن يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ ۙ وَهُوَ عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿٧٦﴾
Na Allaah amepiga mfano (mwingine) wa watu wawili; mmoja ni bubu asiye na uwezo juu ya chochote naye ni mzigo kwa bwana wake, popote unapomuelekeza haleti khayr. Je, analingana sawa yeye na yule anayeamrisha uadilifu, naye yuko juu ya njia iliyonyooka? [An-Nahl: 75-76]
Na aliyekuwa bubu ni mmojawapo kati ya wawili, na aliye mzigo kwa bwana wake ni Asyad bin Abiy Al-‘Iysw. Na yule ambaye anaamrisha uadilifu naye yuko juu ya njia ya kunyooka ni ‘Uthmaan bin ‘Affaan (رضي الله عنه).
[Abul-Hasan ‘Aliy Ibn Ahmad Al-Waahidi An-Naysaaburiy]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
016- Suwrah An-Nahl Aayah: 103
Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):
وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَنَّهُمْ يَقُولُونَ إِنَّمَا يُعَلِّمُهُ بَشَرٌ ۗ لِّسَانُ الَّذِي يُلْحِدُونَ إِلَيْهِ أَعْجَمِيٌّ وَهَـٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيٌّ مُّبِينٌ﴿١٠٣﴾
Na kwa yakini Tunajua kwamba wao wanasema: Hakika hapana isipokuwa mtu anamfundisha (Muhammadصلى الله عليه وآله وسلم Qur-aan). Lugha wanayomnasibishia nayo ni ya kigeni, na hii ni lugha ya Kiarabu bayana. [An-Nahl: 103]
Sababun-Nuzuwl:
عَنْ عَبْد اللَّه بْن مُسْلِم الْحَضْرَمِيّ قال: كَانَ لَنَا غُلَامَانِ نَصْرَانِيَّانِ مِنْ أَهْلِ عَيْنِ التَّمْرِ، اسْمُ أَحَدِهِمَا يَسَارٌ وَاسْمُ الْآخَرِ جَبْرٌ ، وَكَانَا يَقْرَآنِ كِتَابًا لَهُمْ. (التَّوْرَاةَ) فَكَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَمُرُّ بِهِمَا وَيَسْمَعُ قِرَاءَتَهُمَا، وَكَانَ الْمُشْرِكُونَ يَقُولُونَ: يَتَعَلَّمُ مِنْهُمَا، فَأَنْزَلَ اللَّهُ هَذِهِ الْآيَةَ:
لِّسَانُ الَّذِي يُلْحِدُونَ إِلَيْهِ أَعْجَمِيٌّ وَهَـٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيٌّ مُّبِينٌ﴿١٠٣﴾
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Muslim Al-Hadhwramiyy amesema: Tulikuwa na vijana wawili Manaswara kutoka Watu wa ‘Ayn At-Tamar, mmojawapo akiitwa Yasaar na mwenginewe Jabr, na walikuwa wakiwasomea Kitabu (Tawraat) na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akiwapitia na kuwasikia Qiraa chao, basi washirikina wakawa wanasema: “Anajifunza kutoka kwa hao wawili.” Hapo Allaah Akateremsha:
لِّسَانُ الَّذِي يُلْحِدُونَ إِلَيْهِ أَعْجَمِيٌّ وَهَـٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيٌّ مُّبِينٌ﴿١٠٣﴾
Lugha wanayomnasibishia nayo ni ya kigeni, na hii ni lugha ya Kiarabu bayana.
[Qurtwubiy – Jaami’ Ahkaam Al-Qur-aan, Ibn Jariyr]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
016- Suwrah An-Nahl Aayah: 110
Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):
ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِن بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِن بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١١٠﴾
Kisha hakika Rabb wako, kwa wale waliohajiri baada ya kutiwa katika mitihani, kisha wakafanya jihaad na wakasubiri; hakika Rabb wako baada ya hayo bila shaka ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nahl: 110]
Sababun-Nuzuwl:
عن ابن عباس قال: كان قوم من أهل مكة أسلموا وكانوا يستخفون بالإسلام، فأخرجهم المشركون يوم بدر معهم، فأصيب بعضهم وقتل بعض، فقال المسلمون: كان أصحابنا هؤلاء مسلمين وأكرهوا فاستغفروا لهم فنزلت ((إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلائِكَةُ ظَالِمِي أَنْفُسِهِمْ)) إلى آخر الآية. قال: وكتب إلى من بقي بمكة من المسلمين هذه الآية لا عذر لهم قال: فخرجوا فلحقهم المشركون فأعطوهم الفتنة فنزلت هذه الآية ((وَمِنَ النَّاسِ مَنْ يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّهِ جَعَلَ فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّهِ)) إلى آخر الآية. فكتب المسلمون إليهم بذلك فخرجوا وأيسوا من كل خير ثم نزلت فيهم ((ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِنْ بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِنْ بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَحِيمٌ)) فكتبوا إليهم بذلك إن الله قد جعل لكم مخرجا ، فخرجوا فأدركهم المشركون فقاتلوهم ثم نجا من نجا وقتل من قتل.
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba kulikuwepo watu wa Makkah waliosilimu wakawa wanaficha Uislamu wao. Washirikina wakawatoa siku ya vita vya Badr pamoja nao, na wakajeruhiwa baadhi yao na wengineo wakauawa. Waislamu wakasema: “Hawa walikuwa marafiki zetu wa Kiislamu.” Basi walilazimishwa (kutoka kupigana), wakawaombea maghfirah ikateremka:
إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾
Hakika wale ambao Malaika wamewafisha, hali wamejidhulumu nafsi zao; (Malaika) watawaambia: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi. (Malaika) Watasema: Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia [An-Nisaa: 97]
Akasema: Ikatolewa hukumu kwa Waislamu waliobakia Makkah kuwa hawana udhuru kutokana na Aayah hii. Wakatoka, wakakutana na washirikina wakawatia katika fitnah (mitihani) ikateremka Aayah ifuatayo:
وَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّـهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّـهِ جَعَلَ فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّـهِ وَلَئِن جَاءَ نَصْرٌ مِّن رَّبِّكَ لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمْ ۚ أَوَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَعْلَمَ بِمَا فِي صُدُورِ الْعَالَمِينَ ﴿١٠﴾
Na miongoni mwa watu wako wasemao: Tumemwamini Allaah; lakini wanapoudhiwa kwa ajili ya Allaah, hufanya fitnah za watu kama kwamba ni adhabu ya Allaah. Na inapowajia nusura kutoka kwa Rabb wako husema: Hakika sisi tulikuwa pamoja nanyi. Je, kwani Allaah Hayajui yale yaliyomo katika vifua vya walimwengu? [Al-‘Ankabuwt: 10]
Wakaandikiwa hukumu Waislamu kwa hayo, wakatoka na wakaacha kufanya kheri zote ikawateremkia:
ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِن بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِن بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١١٠﴾
Kisha hakika Rabb wako, kwa wale waliohajiri baada ya kutiwa katika mitihani, kisha wakafanya jihaad na wakasubiri; hakika Rabb wako baada ya hayo bila shaka ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nahl: 110]
Wakaandikiwa hukumu kwa hiyo kwamba Allaah Amekujaalieni njia. Wakatoka wakakutana na washirikina wakapigana, na baadhi kuuwawa na baadhi kupona.
[Ibn Jariyr]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
016-Asbaab Nuzuwl An-Nahl Aayah : 126
Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى)
وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُم بِهِ ۖ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ﴿١٢٦﴾
Na mkilipiza, basi lipizeni kulingana na vile mlivyoadhibiwa. Na mkisubiri, basi bila shaka hivyo ni bora kwa wenye kusubiri. [An-Nahl: 126]
Sababun-Nuzuwl:
حَدَّثَنَا أَبُو عَمَّارٍ الْحُسَيْنُ بْنُ حُرَيْثٍ، حَدَّثَنَا الْفَضْلُ بْنُ مُوسَى، عَنْ عِيسَى بْنِ عُبَيْدٍ، عَنِ الرَّبِيعِ بْنِ أَنَسٍ، عَنْ أَبِي الْعَالِيَةِ، قَالَ حَدَّثَنِي أُبَىُّ بْنُ كَعْبٍ، قَالَ لَمَّا كَانَ يَوْمُ أُحُدٍ أُصِيبَ مِنَ الأَنْصَارِ أَرْبَعَةٌ وَسِتُّونَ رَجُلاً وَمِنَ الْمُهَاجِرِينَ سِتَّةٌ فِيهِمْ حَمْزَةُ فَمَثَّلُوا بِهِمْ فَقَالَتِ الأَنْصَارُ لَئِنْ أَصَبْنَا مِنْهُمْ يَوْمًا مِثْلَ هَذَا لَنُرْبِيَنَّ عَلَيْهِمْ قَالَ فَلَمَّا كَانَ يَوْمُ فَتْحِ مَكَّةَ فَأَنْزَلَ اللَّهُ ((وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُمْ بِهِ وَلَئِنْ صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِلصَّابِرِينَ)) فَقَالَ رَجُلٌ: لاَ قُرَيْشَ بَعْدَ الْيَوْمِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم :" كُفُّوا عَنِ الْقَوْمِ إِلاَّ أَرْبَعَةً " . قَالَ هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ غَرِيبٌ مِنْ حَدِيثِ أُبَىِّ بْنِ كَعْبٍ
Ametuhadithia Abuu ‘Ammaar Al-Husayn bin Hurayth, ametuhadithia Al-Fadhwl bin Muwsa kutoka kwa ‘Iysaa bin ‘Ubayd, kutoka kwa Ar-Rabi’y bin Anas, kutoka kwa Abuu Al-‘Aaliyah amesema: amenihadithia Ubayy bin Ka’b ambaye amesema: Siku ya vita vya Uhud, watu sitini na nne katika Answaariy waliuawa, na sita kutoka kwa Muhaajiriyn. Mmoja wao alikuwa ni Hamzah, wakamtumbua basi Answaariy wakasema: “Ikiwa (siku za mbele) tukijaaliwa kupigana nao (tukawaua) siku kama hii, nasi tutawatumbua baadhi yao mara mbili yake (kama walivyowatumbua baadhi yetu).” Akasema: Basi siku ya Fat-h Makkah Allaah Akateremsha:
وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُم بِهِ ۖ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ﴿١٢٦﴾
Na mkilipiza, basi lipizeni kulingana na vile mlivyoadhibiwa. Na mkisubiri, basi bila shaka hivyo ni bora kwa wenye kusubiri. [An-Nahl: 126]
Mtu mmoja akasema: “Hakutakuwa na Quryash tena baada ya leo.” Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Waacheni watu isipokuwa wanne tu.” [At-Tirmidhiy, amesema Hii Hadiyth Hasan Ghariyb katika Hadiyth za Ubayy bin Ka’ab]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/238
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10413&title=016-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20An-Nahl
[4] http://alhidaaya.com
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10414&title=075-Asbaab%20Nuzuwl%3A%20An-Nahl%20Aayah%20075%3A%20%D8%B6%D9%8E%D8%B1%D9%8E%D8%A8%D9%8E%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%91%D9%8E%D9%80%D9%87%D9%8F%20%D9%85%D9%8E%D8%AB%D9%8E%D9%84%D9%8B%D8%A7%20%D8%B9%D9%8E%D8%A8%D9%92%D8%AF%D9%8B%D8%A7%20%D9%85%D9%91%D9%8E%D9%85%D9%92%D9%84%D9%8F%D9%88%D9%83%D9%8B%D8%A7%20%D9%84%D9%91%D9%8E%D8%A7%20%D9%8A%D9%8E%D9%82%D9%92%D8%AF%D9%90%D8%B1%D9%8F%20%D8%B9%D9%8E%D9%84%D9%8E%D9%89%D9%B0%20%D8%B4%D9%8E%D9%8A%D9%92%D8%A1%D9%8D%20%D9%88%D9%8E%D9%85%D9%8E%D9%86%20%D8%B1%D9%91%D9%8E%D8%B2%D9%8E%D9%82%D9%92%D9%86%D9%8E%D8%A7%D9%87%D9%8F%20
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10415&title=103-Asbaab%20Nuzuwl%3A%20An-Nahl%20Aayah%20103%3A%20%D9%88%D9%8E%D9%84%D9%8E%D9%82%D9%8E%D8%AF%D9%92%20%D9%86%D9%8E%D8%B9%D9%92%D9%84%D9%8E%D9%85%D9%8F%20%D8%A3%D9%8E%D9%86%D9%91%D9%8E%D9%87%D9%8F%D9%85%D9%92%20%D9%8A%D9%8E%D9%82%D9%8F%D9%88%D9%84%D9%8F%D9%88%D9%86%D9%8E%20%D8%A5%D9%90%D9%86%D9%91%D9%8E%D9%85%D9%8E%D8%A7%20%D9%8A%D9%8F%D8%B9%D9%8E%D9%84%D9%90%D9%91%D9%85%D9%8F%D9%87%D9%8F%20%D8%A8%D9%8E%D8%B4%D9%8E%D8%B1%D9%8C%20%DB%97%20%D9%84%D9%90%D9%91%D8%B3%D9%8E%D8%A7%D9%86%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D9%91%D9%8E%D8%B0%D9%90%D9%8A%20%D9%8A%D9%8F%D9%84%D9%92%D8%AD%D9%90%D8%AF%D9%8F%D9%88%D9%86%D9%8E%20%D8%A5%D9%90%D9%84%D9%8E%D9%8A%D9%92%D9%87%D9%90%20%D8%A3%D9%8E%D8%B9%D9%92%D8%AC%D9%8E%D9%85%D9%90%D9%8A%D9%91%D9%8C%20
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10416&title=110-Asbaab%20Nuzuwl%3A%20An-Nahl%20Aayah%20110%3A%20%D8%AB%D9%8F%D9%85%D9%91%D9%8E%20%D8%A5%D9%90%D9%86%D9%91%D9%8E%20%D8%B1%D9%8E%D8%A8%D9%91%D9%8E%D9%83%D9%8E%20%D9%84%D9%90%D9%84%D9%91%D9%8E%D8%B0%D9%90%D9%8A%D9%86%D9%8E%20%D9%87%D9%8E%D8%A7%D8%AC%D9%8E%D8%B1%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D9%85%D9%90%D9%86%20%D8%A8%D9%8E%D8%B9%D9%92%D8%AF%D9%90%20%D9%85%D9%8E%D8%A7%20%D9%81%D9%8F%D8%AA%D9%90%D9%86%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D8%AB%D9%8F%D9%85%D9%91%D9%8E%20%D8%AC%D9%8E%D8%A7%D9%87%D9%8E%D8%AF%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D9%88%D9%8E%D8%B5%D9%8E%D8%A8%D9%8E%D8%B1%D9%8F%D9%88%D8%A7
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10417&title=126-Asbaab%20Nuzuwl%3A%20An-Nahl%20Aayah%20126%3A%20%D9%88%D9%8E%D8%A5%D9%90%D9%86%D9%92%20%D8%B9%D9%8E%D8%A7%D9%82%D9%8E%D8%A8%D9%92%D8%AA%D9%8F%D9%85%D9%92%20%D9%81%D9%8E%D8%B9%D9%8E%D8%A7%D9%82%D9%90%D8%A8%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D8%A8%D9%90%D9%85%D9%90%D8%AB%D9%92%D9%84%D9%90%20%D9%85%D9%8E%D8%A7%20%D8%B9%D9%8F%D9%88%D9%82%D9%90%D8%A8%D9%92%D8%AA%D9%8F%D9%85%20%D8%A8%D9%90%D9%87%D9%90%20%DB%96%20%D9%88%D9%8E%D9%84%D9%8E%D8%A6%D9%90%D9%86%20%D8%B5%D9%8E%D8%A8%D9%8E%D8%B1%D9%92%D8%AA%D9%8F%D9%85%D9%92%20%D9%84%D9%8E%D9%87%D9%8F%D9%88%D9%8E%20%D8%AE%D9%8E%D9%8A%D9%92%D8%B1%D9%8C%20%D9%84%D9%90%D9%91%D9%84%D8%B5%D9%91%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%90%D8%B1%D9%90%D9%8A%D9%86%D9%8E