200 سُؤالٌ وَ جَوَابٌ فِي الْعَقِيدَة
Maswali 200 Na Majibu Ya ‘Aqiydah
لِلشَّيخ حافِظ بن أحْمَد الحَكمَيّ
Shaykh Haafidhw Bin Ahmad Al-Hakamiyy (رحمه الله)
Imefasiriwa na: Alhidaaya.com [1]
016-Ni Ipi Nafasi Ya Shahaadah Mbili Katika Dini?
Swali:
س: ما محل الشهادتين من الدين
Ni ipi nafasi ya shahaadah mbili katika Dini?
Jibu:
ج: لا يدخل العبد في الدين إلا بهما
قال الله تعالى ( إنما المؤمنون الذين آمنوا بالله ورسوله )
وقال النبي صلى الله عليه وسلم ( أمرت أن أقاتل الناس حتى يشهدوا أن لا إله إلا الله وأن محمدا عبده ورسوله ) الحديث وغير ذلك كثير.
Mtu haingii katika Dini isipokuwa kwa Shahaadah hizo mbili. Allaah Anasema:
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ
Hakika Waumini ni wale waliomwamini Allaah na Rasuli Wake [An-Nuwr (24: 62)]
Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema:
((أُمِرْتُ أن أقاتِل الناسَ حتى يَشهدُوا أن لا إله إلا الله ، أنَّ محمداً رسولُ الله...)
((Nimeamrishwa kupigana na watu mpaka washuhudie kuwa hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah na kwamba Muhammad ni Rasuli Wake)) [Al-Bukhariy na Muslim Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin ‘Umar (رضي الله عنهما)]
Na Hadiyth nyenginezo zaidi ya hiyo.
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10737&title=016-Maswali%20200%20Na%20Majibu%20Ya%20%E2%80%98Aqiydah%3A%20Ni%20Ipi%20Nafasi%20Ya%20Shahaadah%20Mbili%20Katika%20Dini%3F