Hadiyth: Fadhila Za ‘Ilmu Na ‘Ulamaa
Hadiyth Ya 18
Allaah Huichukua ‘Ilmu Kwa Kufariki ‘Ulamaa
Kisha Viongozi Wajinga Watatoa Fatwa Bila ‘Ilmu
Alhidaaya.com [1]
عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ، قَالَ سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ " إِنَّ اللَّهَ لاَ يَقْبِضُ الْعِلْمَ انْتِزَاعًا، يَنْتَزِعُهُ مِنَ الْعِبَادِ، وَلَكِنْ يَقْبِضُ الْعِلْمَ بِقَبْضِ الْعُلَمَاءِ، حَتَّى إِذَا لَمْ يُبْقِ عَالِمًا، اتَّخَذَ النَّاسُ رُءُوسًا جُهَّالاً فَسُئِلُوا، فَأَفْتَوْا بِغَيْرِ عِلْمٍ، فَضَلُّوا وَأَضَلُّوا ".
Abdallaaah bin Amr bin Al-Aasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesimulia: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Allaah Haiondoshi ‘Ilmu kwa kuichukua kutoka kwa (mioyo ya) watu, lakini Huichukua kwa kufariki ‘Ulamaa mpaka watakapokwisha (‘Ulamaa) wote, watu watachukua kama wao viongozi wajinga ambao wataulizwa na watatoa Fatwa bila ‘Ilmu. Kwa hiyo watapotoka na watapotosha (Ummah). [Al-Bukhaariy, Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10900&title=18-Hadiyth%3A%20Fadhila%20Za%20%27Ilmu%20Na%20%27Ulamaa%3A%20Allaah%20Huichukua%20%E2%80%98Ilmu%20Kwa%20Kufariki%20%E2%80%98Ulamaa%20Kisha%20Viongozi%20Wajinga%20Watatoa%20Fatwa%20Bila%20%E2%80%98Ilmu