Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النّهي عن القِرَانِ بين تمرتين ونحوهما إِذَا أكل جماعة إِلاَّ بإذن رفقته
06-Mlango Wa Unaokataza Kubana Tende Mbili na Mfano Wake Katika Tonge Moja Kama Anakula na Wenzake Isipokuwa Kwa Ruhusa Yao
Alhidaaya.com [1]
عن جَبَلَة بن سُحَيْم ، قَالَ : أصَابَنَا عَامُ سَنَةٍ مَعَ ابن الزُّبَيْرِ ؛ فَرُزِقْنَا تَمْراً، وَكَانَ عبدُ الله بن عمر رضي الله عنهما يَمُرُّ بنا ونحن نَأكُلُ، فَيقُولُ : لاَ تُقَارِنُوا ، فإنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم نَهَى عنِ القِرَانِ ، ثُمَّ يَقُولُ : إِلاَّ أنْ يَسْتَأذِنَ الرَّجُلُ أخَاهُ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Jabalah bin Suhaym kwamba: Tulipatikana na ukame mwaka mmoja tukiwa pamoja na Ibn Zubayr, naye akawa anatupa tende na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) alikuwa anatupitia tukiwa tunakula na kusema: "Musibane tende, hakika Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kubana, kula tende mbili kwa mlo mmoja." Kisha akasema: "Isipokuwa mtu miongoni mwenu atakapomuomba ruhusa ndugu yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10965&title=06-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Unaokataza%20Kubana%20Tende%20Mbili%20na%20Mfano%20Wake%20Katika%20Tonge%20Moja%20Kama%20Anakula%20na%20Wenzake%20Isipokuwa%20Kwa%20Ruhusa%20Yao