Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الموعظة عند القبر
17-Mlango Wa Mawaidha Kwenye Kaburi
Alhidaaya.com [1]
عن عَلِيٍّ رضي الله عنه ، قَالَ : كُنَّا فِي جَنَازَةٍ في بَقيعِ الغَرْقَدِ ، فَأتَانَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم فَقَعَدَ ، وَقَعَدْنَا حَوْلَهُ وَمَعَهُ مِخْصَرَةٌ فَنَكَّسَ وَجَعَلَ يَنْكُتُ بِمِخْصَرَتِهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( مَا مِنْكُمْ مِنْ أحَدٍ إِلاَّ وَقَدْ كُتِبَ مَقْعَدُهُ مِنَ النَّارِ وَمَقْعَدُهُ مِنَ الجَنَّةِ )) فقالوا : يَا رسولَ الله ، أفَلا نَتَّكِلُ عَلَى كِتَابنَا ؟ فَقَالَ : (( اعْمَلُوا ؛ فكلٌّ مُيَسرٌ لِمَا خُلِقَ لَهُ ... )) وذكَر تَمَامَ الحديث . متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa na jeneza makaburi ya Baqi' Al-Gharqad. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatujia akakaa, tukakaa pembeni yake akiwa na bakora, Akainamisha kichwa chake na anakwaruza ardhi kwa fimbo yake. Kisha akasema: "Hakuna yoyote miongoni mwenu ila ameandikiwa kikao chake motoni na kikao chake Peponi." Wakauliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Tutegemee katika vitabu vyetu?", Akasema: "Fanyeni kwani kila mmoja amerahisishiwa alioumbiwa (na kukuduriwa)." Na akataja Hadiyth hiyo kwa ukamilifu wake. [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11066&title=17-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Mawaidha%20Kwenye%20Kaburi