Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: [1]
Hadiyth Ya 31
ازْهَدْ فِي الدُّنْيَا يُحِبُّكَ اللَّهُ
Ipe Mgongo Dunia Allaah Atakupenda
Alhidaaya.com [2]
عَنْ أَبِي العَبّاسِ سَهلِ بْن سَعْدٍ السّاعِدِيِّ رضي الله عنه قَالَ : جَاءَ رَجُلُ إِلى النَبِي صلى الله عليه وسلم فَقَالَ : يَا رَسُولَ اللَّهِ دُلَّنِي عَلَى عَمَلٍ إِذَا عَمِلْتُهُ أَحَبَّنِي اللَّهُ وَأَحَبَّنِي النَّاسُ . فَقَالَ: (( ازْهَدْ فِي الدُّنْيَا يُحِبُّكَ اللَّهُ وَازْهَدْ فِيمَا عِنْدَ النَّاسِ يُحِبُّكَ النّاسُ)) رَوَاهُ ابْنُ مَاجَهْ وَغَيْرُهُ بِأَسَانِيدَ حَسَنَةٍ.
Imepokelewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad As-Saa’idiyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: “Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nijulishe ‘amali ambayo nikiifanya Allaah Atanipenda na watu pia watanipenda. Akasema: “Ipe mgongo dunia Allaah Atakupenda, na vipe mgongo vilivyomo kwa watu, watu watakupenda.” [Ibn Maajah na wengineo kwa mtiririko mzuri wa isnaad]*
*Hata hivyo Wanavyuoni wa Hadiyth wameeleza kuwa Hadiyth hii ni dhaifu kutokana na udhaifu wa sanad yake japo An-Nawawiy kaitumia na kasema ina sanad nzuri.
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/node/961
[2] http://www.alhidaaya.com/
[3] http://www.alhidaaya.com/swahili/hadiyth/Hadiyth%2040%20An-Nawawiy/31-Ipe%20Mgongo%20Dunia%20Allaah%20Atakupenda.mp3
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F1291&title=31-Al-Arba%E2%80%99uwn%20An-Nawawiyyah%3A%20Ipe%20Mgongo%20Dunia%20Allaah%20Atakupenda