Zakaatu-Fitwr Apewe Nani?
Al-Lajnah Ad-Daaimah
SWALI
Zakaatul-Fitwr apewe nani? Je, inaruhusiwa kuituma mfano kwa Mujaahidiyn waliko vitani? Au kuitoa katika vyama vinavyokusanya sadaka au kujengea msikiti?
JIBU:
AlhamduliLLaah
Zakaatul-Fitwr inapaswa kupewa maskini Waislamu katika nchi au mji ambao inatolewa kwa sababu ya usimulizi wa Abuu Daawuwd kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha Zakaatul-Fitwr ilipwe Ramadhwaan kuwalisha watu masikini…."
Inaruhusiwa kuituma kwa masikini wa nchi nyingine ambao watu wake wanahitaji zaidi. Hairuhusiwi kujengea msikiti au kuitoa katika miradi ya sadaka.
[Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F1921&title=02-Al-Lajnah%20Ad-Daaimah%3A%20Zakaatul-Fitwr%20%20Apewe%20Nani%3F