Hukmu Ya Kukanusha Zakaatul-Fitwr
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)
SWALI:
Nini hukmu ya kukanusha Zakaatul-Fitwr na vipi ahukumiwe mwenye kuikanusha?
JIBU:
Kuikanusha hairuhusiwi (haraam) kwa sababu itakuwa ni kupinga aliyoamrisha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyokwishatajwa katika Hadiyth ya 'Ibn 'Umar ambaye amesema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alifaridhisha Zakaatul-Fitw…" Na inajulikana kwamba kuacha kutenda kilichofaridhishwa hairuhusiwi (ni haraam) na (kufanya hivyo) ni dhambi na kuasi (amri)
[Imaam Ibn ‘Uthaymiyn Fataawaa Ramadhwaan – Mjalada 2, Uk. 902, Fatwa Namba 887- Fiqhul-'Ibaadaati libni 'Uthaymiyn – Uk. 213]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F1959&title=26-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthaymiyn%3A%20Hukmu%20Ya%20Kukanusha%20Zakaatul-Fitwr%20