Kutoa Zakaah: Kutoa Panapowajibika
Alhidaaya.com [1]
Inawajibika kuitoa Zakaah wakati wake unapowadia, na haijuzu kuichelewesha isipokuwa kwa dharura inayokubalika.
Kutoka kwa Bibi ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema kuwa; Nabiy (Swalla Alaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
"Haichanganyiki mali pamoja na Zakaah isipokuwa itaiangamiza", na katika riwaya nyingine;
"Inakuwa ishakuwajibikia katika mali yako kuitolea Zakaah, kisha usiitoe, kwa hivyo (mali ya) haramu (isiyotolewa Zakaah) inaiangamiza (mali ya) halali". [Ash-Shaafi’iy na Al-Bukhaariy katika 'At-Taariykh']
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F4623&title=015-Kutoa%20Zakaah%3A%20Kutoa%20Panapowajibika