الشَّرْح
094-Ash-Sharh
094-Ash-Sharh: Utangulizi Wa Suwrah [1]
Alhidaaya.com [2]
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
أَلَمْ نَشْرَحْ لَكَ صَدْرَكَ ﴿١﴾
1. Je, kwani Hatukukunjulia kifua chako kukubainishia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)?
وَوَضَعْنَا عَنكَ وِزْرَكَ ﴿٢﴾
2. Na Tukakuondolea mzigo wako (wa dhambi)?
الَّذِي أَنقَضَ ظَهْرَكَ ﴿٣﴾
3. Ambao ulielemea mgongo wako?
وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ ﴿٤﴾
4. Na Tukakutukuzia kutajwa kwako?
فَإِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا ﴿٥﴾
5. Basi hakika pamoja na kila ugumu kuna wepesi.
إِنَّ مَعَ الْعُسْرِ يُسْرًا ﴿٦﴾
6. Hakika pamoja na kila ugumu kuna wepesi.
فَإِذَا فَرَغْتَ فَانصَبْ ﴿٧﴾
7. Basi utakapopata faragha fanya juhudi katika ibaada.
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَارْغَب ﴿٨﴾
8. Na kwa ajili ya Rabb wako, ongeza utashi zaidi (wa ibaada).
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/node/11600
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7082&title=094%20-%20Ash-Sharh