Du’aa Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
Kuomba Mema Ya Duniani Na Aakhirah Na Kinga Ya Adhabu Ya Moto
Alhidaaya.com [1]
Hii ni miongoni mwa du'aa alizokuwa akiomba sana Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).
رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الأَخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ
Rabbaana aatinaa fid-dduniya hasanatan wafil Aakhirati hasanatan wa qinaa adhaaban-naari
Rabb wetu, tupe katika dunia mema na katika Akhera mema na Tukinge adhabu ya moto [Hadiyth ya Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu kwamba ilikuwa miongoni mwa du'aa alizokithirisha kuziomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Al-Bukhaariy, Muslim]
Faida: Du’aa hii ni ambayo imejumuisha maana nyingi ndani yake kwa kuwa imehusisha kuomba mema ya dunia na Aakhirah. Na Du’aa hii inapatikana pia ndani ya Qur-aan Suwratul Baqarah (2: 201]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7962&title=001-Du%27aa%20Za%20Nabiy%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%3A%20Mema%20Ya%20Duniani%20Na%20Aakhirah%20Na%20Kinga%20Ya%20Adhabu%20Ya%20Moto