Aayah Na Mafunzo
Aal-‘Imraan
Makabila Mawili Kufurahia Kuteremshwa Na Allaah Ni Mlinzi Wao
إِذْ هَمَّت طَّائِفَتَانِ مِنكُمْ أَن تَفْشَلَا وَاللَّـهُ وَلِيُّهُمَا ۗ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١٢٢﴾
122. Pale walipofanya wasiwasi makundi mawili miongoni mwenu kwamba watashindwa na Allaah ni Mlinzi na Msaidizi wao; basi kwa Allaah pekee na watawakali Waumini.
Mafunzo:
Sababun-Nuzuwl:: Aayah hii imeteremka ikiwazungumzia Banuw Salamah na Banuw Haarithah kama alivyohadhithia Jaabir (رضي الله عنه) kwamba: Aayah hii imeteremshwa kuhusu sisi nasi tulikuwa ni makabila mawili; Banuw Haarithah na Banuw Salamah tusingelipenda (kama isingeteremshwa) na Sufyaan kasema: Tusingefurahi kama isingeteremshwa na hali Allaah Anasema: “Na Allaah ni Mlinzi na Msaidizi wao.” [Amehadithia Jaabir (رضي الله عنه) ameipokea Al-Bukhaariy na Muslim].
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8150&title=122-Aayah%20Na%20Mafunzo%3A%20Makabila%20Mawili%20Kufurahia%20Kuteremshwa%20Na%20Allaah%20Ni%20Mlinzi%20Wao