Kufuturu Tende Kwa Idadi Ya Witr
Imaam Ibn ‘Uthyamiyn (Rahimahu-Allaah)
SWALI:
Nimesikia kwammba mwenye swawm anawajibika pale anapofuturu tende, iwe ni idadi ya witr yaani iwe tano au saba na kadhaalika Je ni waajib?
JIBU:
Si waajib, bali hata sio Sunnah mtu afuturu kwa witr; tatu au tano au saba au tisa isipokuwa Siku ya ‘Iyd kwani imethibiti kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa hatoki kwenda Swalaah Siku ya ‘Iydul-Fitwr mpaka ale kwanza tamar (tende) na alikuwa akila kwa witr.
Ama nje ya hayo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakukusudia kula tende kwa witr.
[Fataawa Nuwr ‘Alad-Darb 11/2]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8404&title=02-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthyamiyn%3A%20Kufuturu%20Tende%20Kwa%20Idadi%20Ya%20Witr