Israfu Ya Chakula Wakati Wa Futari
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)
SWALI:
Je, mtu hupata thawabu ndogo (ya Swawm) ikiwa atakithirisha kukata Swawm (Futari) kwa masahani ya vyakula mbali mbali?
JIBU:
Hapana, hupati thawabu ndogo ya Swawm. Mtu kufanya kitendo cha haraam baada ya kumaliza Swawm, (kitendo kile) hakiathiri thawabu (za Swawm). Bali inaingia katika neno Lake Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
وَكُلُوا وَاشْرَبُوا وَلَا تُسْرِفُوا ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُسْرِفِينَ ﴿٣١﴾
“Na kuleni na kunyweni; na wala msifanye israfu. Hakika Yeye (Allaah) Hapendi wanaofanya israfu. [Al-A’raaf 7: 31]
Huku kufanya israfu ndiyo haraam. Na iktisadi ni nusu ya maisha. Ikiwa bila kukusudia kutabaki chakula, ni afadhali kitolewe swadaqah.
[Fiqhu Al-'Ibaadah, uk. 252]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8408&title=01-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthaymiyn%3A%20Israfu%20Ya%20Chakula%20Wakati%20Wa%20Futari