Akimeza Maji Bila Kukusudia Kutokana Na Kusukutua Swawm Yake Inabatilika?
Imaam Ibn ‘Uthyamiyn (Rahimahu Allaah)
SWALI:
Je, Swawm ya mfungaji inabatilika ikiwa atasukutua kinywa au pua na kwa bahati mbaya akameza maji?
JIBU:
Aliyekuwa katika swawm akaukutua kinywa au pua na maji yakamuingia, Swawm yake haibatiliki, kwa kuwa hakukusudia hilo. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:
وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ ۚ
lakini isipokuwa katika yale yaliyoyakusudia nyoyo zenu [Al-Ahzaab 33;5]
[Imaam Muhammad Swaalih Ibn 'Uthaymiyn - Fiqhul-'Ibaadat, uk. 253]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8451&title=07-Imaam%20Ibn%20%E2%80%98Uthyamiyn%3A%20Akimeza%20Maji%20Bila%20Kukusudia%20Kutokana%20Na%20Kusukutua%20Swawm%20Yake%20Inabatilika%3F