Sifa Ya Swalaah Ya ‘Iyd
Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)
Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:
i-Inaletwa Takbiyrah Al-Ihraam na inafunguliwa kwa du’aa kisha zinaletwa Takbiyrah sita (jumla zitakuwa saba) kisha inasomwa Al-Faatihah na Suwrah ima (Sabbihisma) au (Qaaf) katika Raka’ah ya kwanza.
ii-Katika Raka’ah ya pili, atakaposimama kutoka katika kusujudu, atainuka huku akileta Takbiyrah kisha ataleta Takbiyrah tano baada ya kusimama kwake. Kisha atasoma Al-Faatihah na Suwrah. Ikiwa atasoma katika Rakaa ya kwanza (Sabbihismaa) basi asome katika Rakaa ya pili (Al-Ghaashiyah). Na pindi akiwa amesoma katika Rakaa ya kwanza (Qaaf), basi asome katika Rakaa ya pili (Iqtarabatis-Saa’ah .. Suwrah Al-Qamar)
[Majmuw’ Al-Fataawaa (16/223)]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8643&title=03-Imaam%20Ibn%20%27Uthaymiyn%3A%20Sifa%20Ya%20Swalaah%20Ya%20%E2%80%98Iyd