Sababu Za Kuteremshwa
(Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Suwrah Al-A’raaf
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [2]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
031: Enyi wana wa Aadam! Chukueni mapambo yenu (ya mavazi ya sitara na twahara) katika kila mahala pa ‘Ibaadah.
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
يَا بَنِي آدَمَ خُذُوا زِينَتَكُمْ عِندَ كُلِّ مَسْجِدٍ وَكُلُوا وَاشْرَبُوا وَلَا تُسْرِفُوا ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الْمُسْرِفِينَ ﴿٣١﴾
Enyi wana wa Aadam! Chukueni mapambo yenu (ya mavazi ya sitara na twahara) katika kila mahala pa ‘Ibaadah. Na kuleni na kunyweni na wala msifanye israfu. Hakika Yeye (Allaah) Hapendi wanaofanya israfu. [Al-A’raaf (7:31)]
Sababun-Nuzwul:
Sa’iyd bin Jubayr amehadithia kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kwamba Washirikina wanawake na wanaume walikuwa wakitufu Al-Ka’bah. Wanaume wakitufu mchana na wanawake wakitufu usiku. Wanawake wakisema wanapotufu: Leo baadhi yake (uchi) au wote uonekane na kitakachoonekana sikitolei ruhusa. Hapo ikateremka:
يَا بَنِي آدَمَ خُذُوا زِينَتَكُمْ عِندَ كُلِّ مَسْجِدٍ
Enyi wana wa Aadam! Chukueni mapambo yenu (ya mavazi ya sitara na twahara) katika kila mahala pa ‘Ibaadah. [Al-A’raaf (7:31)]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
Al-A’raaf 175
175-Na wasomee (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) khabari za yule Tuliyempa Aayaat (ishara, dalili) Zetu, akajivua nazo na shaytwaan akamfuata, na akawa miongoni mwa waliopotoka.
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ الَّذِي آتَيْنَاهُ آيَاتِنَا فَانسَلَخَ مِنْهَا فَأَتْبَعَهُ الشَّيْطَانُ فَكَانَ مِنَ الْغَاوِينَ ﴿١٧٥﴾
Na wasomee (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) khabari za yule Tuliyempa Aayaat (ishara, dalili) Zetu, akajivua nazo na shaytwaan akamfuata, na akawa miongoni mwa waliopotoka.
وَلَوْ شِئْنَا لَرَفَعْنَاهُ بِهَا وَلَـٰكِنَّهُ أَخْلَدَ إِلَى الْأَرْضِ وَاتَّبَعَ هَوَاهُ ۚ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ الْكَلْبِ إِن تَحْمِلْ عَلَيْهِ يَلْهَثْ أَوْ تَتْرُكْهُ يَلْهَث ۚ ذَّٰلِكَ مَثَلُ الْقَوْمِ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا ۚ فَاقْصُصِ الْقَصَصَ لَعَلَّهُمْ يَتَفَكَّرُونَ ﴿١٧٦﴾
Na lau Tungelitaka Tungelimnyanyua kwazo (hizo Aayaat), lakini aligandamana na dunia na akafuata hawaa zake. Basi mfano wake ni kama mfano wa mbwa, ukimhujumu ananing’iniza ulimi nje na kuhema, na ukimwacha pia ananing’iniza ulimi nje na kuhema. Hivyo ndiyo mfano wa watu waliokadhibisha Aayaat Zetu. Basi simulia visa huenda wakatafakari.
سَاءَ مَثَلًا الْقَوْمُ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا وَأَنفُسَهُمْ كَانُوا يَظْلِمُونَ ﴿١٧٧﴾
Uovu ulioje mfano wa watu waliokadhibisha Aayaat Zetu na wakawa wanajidhulumu nafsi zao! [Al-A’raaf (7:175-177)]
Sababun-Nuzuwl:
Mja Aliyepewa Siri Ya Jina Tukufu Kabisa La Allaah (سبحانه وتعالى) Lakini Alifuata Shaytwaan Akapotoka.
Aayah hii na zinazofuatia (7:175-177) zimeteremshwa kuhusu kisa cha Bal’aam ibn Baa’uwraa katika kizazi cha Bani Israaiyl. Alijaaliwa kuwa na ‘Ilmu ya hali ya juu na akajulishwa Jina t Tukufu kabisa la Allaah (سبحانه وتعالى). Lakini akapotoka kwa sababu ya kufuata matamanio na anasa za dunia. Baada ya kushawishiwa na waovu, alikubali kuomba Du’aa dhidi ya Nabiy Muwsaa (عليه السلام) kwa ajili ya kuchuma maslahi ya kidunia. Riwaaya nyengine inasema zimeteremka kumhusu Umayyah bin Abi Asw-Swalt. Riwaayah nyingine ni mtu kutoka Yemen aliyeitwa Bal’am. [Tafsiyr Ibn Kathiyr]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/238
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8997&title=007-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-A%27raaf
[4] http://alhidaaya.com
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8998&title=031-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-A%27raaf%20Aayah%20031%3A%20%20%D9%8A%D9%8E%D8%A7%20%D8%A8%D9%8E%D9%86%D9%90%D9%8A%20%D8%A2%D8%AF%D9%8E%D9%85%D9%8E%20%D8%AE%D9%8F%D8%B0%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D8%B2%D9%90%D9%8A%D9%86%D9%8E%D8%AA%D9%8E%D9%83%D9%8F%D9%85%D9%92%20%D8%B9%D9%90%D9%86%D8%AF%D9%8E%20%D9%83%D9%8F%D9%84%D9%90%D9%91%20%D9%85%D9%8E%D8%B3%D9%92%D8%AC%D9%90%D8%AF%D9%8D%20%D9%88%D9%8E%D9%83%D9%8F%D9%84%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D9%88%D9%8E%D8%A7%D8%B4%D9%92%D8%B1%D9%8E%D8%A8%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D9%88%D9%8E%D9%84%D9%8E%D8%A7%20%D8%AA%D9%8F%D8%B3%D9%92%D8%B1%D9%90%D9%81%D9%8F%D9%88%D8%A7
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8999&title=175-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-A%27raaf%20Aayah%20175%3A%20%20%D9%88%D9%8E%D8%A7%D8%AA%D9%92%D9%84%D9%8F%20%D8%B9%D9%8E%D9%84%D9%8E%D9%8A%D9%92%D9%87%D9%90%D9%85%D9%92%20%D9%86%D9%8E%D8%A8%D9%8E%D8%A3%D9%8E%20%D8%A7%D9%84%D9%91%D9%8E%D8%B0%D9%90%D9%8A%20%D8%A2%D8%AA%D9%8E%D9%8A%D9%92%D9%86%D9%8E%D8%A7%D9%87%D9%8F%20%D8%A2%D9%8A%D9%8E%D8%A7%D8%AA%D9%90%D9%86%D9%8E%D8%A7%20%D9%81%D9%8E%D8%A7%D9%86%D8%B3%D9%8E%D9%84%D9%8E%D8%AE%D9%8E%20%D9%85%D9%90%D9%86%D9%92%D9%87%D9%8E%D8%A7%20%D9%81%D9%8E%D8%A3%D9%8E%D8%AA%D9%92%D8%A8%D9%8E%D8%B9%D9%8E%D9%87%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D8%B4%D9%91%D9%8E%D9%8A%D9%92%D8%B7%D9%8E%D8%A7%D9%86%D9%8F