Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah
36-Kutamka Laa Ilaaha Illa-Allaah Wakati Wa Mafazaiko
عَنْ زَيْنَبَ بِنْتِ جَحْشٍ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم دَخَلَ عَلَيْهَا فَزِعًا يَقُولُ: ((لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، وَيْلٌ لِلْعَرَبِ مِنْ شَرٍّ قَدِ اقْتَرَبَ، فُتِحَ الْيَوْمَ مِنْ رَدْمِ يَأْجُوجَ وَمَأْجُوجَ مِثْلُ هَذَا)) وَحَلَّقَ بِإِصْبَعِهِ وَبِالَّتِي تَلِيهَا، فَقَالَتْ زَيْنَبُ فَقُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ أَنَهْلِكُ وَفِينَا الصَّالِحُونَ؟ قَالَ: ((نَعَمْ، إِذَا كَثُرَ الْخَبَثُ))
Imepokelewa kutoka kwa Zaynba Bint Jahsh (رضي الله عنها) kwamba Nabiy alingia chumbani kwake akiwa katika hali ya kufazaika akasema:
لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ
((Laa ilaaha illa Allaah [hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah]
Ole kwa Waarabu kutokana na shari iliyokaribia. Leo limefunguka shimo katika boma la kizuzi cha Ya-ajuwj na Ma-ajuwj kama hivi!)) Akafanya kiduara kwa kufunga kidole chake cha gumba na cha shahada. Zaynab akasema: Kisha nikasema: Ee Rasuli wa Allaah, hivi tutaangamia na hali tumo watu wema?”. Akasema: ((Ndio pindi maovu yakizidi)) [Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/181) [3346], Muslim (4/2208) [2880] na Riwaayah nyengine: “Aliamka usingizini akasema….
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9351&title=36-Fadhila%20Za%20Laa%20Ilaaha%20Illa-Allaah%3A%20Kutamka%20Laa%20Ilaaha%20Illa-Allaah%20Wakati%20Wa%20Mafazaiko%20%20