أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
(Sababu Za Kuteremshwa Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [2]
028-Asbaab Nuzuwl Al-Qaswasw Aayah 51
Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):
وَلَقَدْ وَصَّلْنَا لَهُمُ الْقَوْلَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٥١﴾
51. Na kwa yakini Tumewafuatilishia na kuwateremshia sehemu kwa sehemu ya Neno ili wapate kukumbuka. [Al-Qaswas (28:51)]
Sababun-Nuzuwl:
Ibn Jariyr katika Mujallaad wa 20 ukurasa wa 88 amesema: “Amenihadithia Bishr bin Aadam amesema, ametuhadithia ‘Affaan bin Muslim amesema, ametuhadithia Hammaad bin Salamah amesema, ametuhadithia ‘Amri bin Diynaar toka kwa Yahyaa bin Ja-’adah amesema: Aayah hii iliteremka kuwazungumzia watu kumi mimi nikiwa mmoja wao:
وَلَقَدْ وَصَّلْنَا لَهُمُ الْقَوْلَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ
Na kwa yakini Tumewafuatilishia na kuwateremshia sehemu kwa sehemu ya Neno ili wapate kukumbuka. [Al-Qaswas (28:51)]
[Hadiyth hii imekharijiwa na At-Twabaraaniy katika Mujallaad wa Tano kurasa za 46 na 47. Al-Haythamiy amesema katika Majma’u Az Zawaaid Mujallaad wa Saba ukurasa wa 88 kuwa imesimuliwa na At-Twabaraaniy kwa Isnaad Mbili; moja ikiwa Muttaswil na wapokezi wake ni watu wa kuaminika, nayo ni hii, na nyingine yenye Isnaad iliyokatika]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/238
[2] http://alhidaaya.com
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11660&title=028-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-Qaswasw%3A%20Aayah%20%2851%29%3A%20%D9%88%D9%8E%D9%84%D9%8E%D9%82%D9%8E%D8%AF%D9%92%20%D9%88%D9%8E%D8%B5%D9%91%D9%8E%D9%84%D9%92%D9%86%D9%8E%D8%A7%20%D9%84%D9%8E%D9%87%D9%8F%D9%85%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D9%92%D9%82%D9%8E%D9%88%D9%92%D9%84%D9%8E%20%D9%84%D9%8E%D8%B9%D9%8E%D9%84%D9%91%D9%8E%D9%87%D9%8F%D9%85%D9%92%20%D9%8A%D9%8E%D8%AA%D9%8E%D8%B0%D9%8E%D9%83%D9%91%D9%8E%D8%B1%D9%8F%D9%88%D9%86%D9%8E%20