Skip navigation.
Home kabah

Nasiha Ya Ijumaa

Fadhila Za Kumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم

Allaah سبحانه وتعالى Anasema,

(( إِنَّ اللَّهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا))  

((Hakika Allaah na Malaika Wake Wanamswalia Nabii, Enyi mlioamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu)) [ Al-Ahzaab:56]

Hii ni amri kutoka kwa Allaah سبحانه وتعالى tumswalie Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na juu ya hivyo kuna fadhila kubwa kumswalia kwake kama ilivyothibiti katika Hadiythi nyingi zifuatazo:

 عنْ عبد اللَّه بن عمرو بن العاص ، رضي اللَّه عنْهُمَا أنَّهُ سمِع رسُول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقُولُ : (( من صلَّى عليَّ صلاَةً ، صلَّى اللَّه علَيّهِ بِهَا عشْراً))   رواهُ مسلم

Imetoka kwa 'Abdullaah bin 'Amru bin Al'-Aasw رضي اللَّه عنْهُمَا kwamba kamsikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم anasema, ((Atakayeniswalia (atakayeniombea)mara moja Allaah Atamswalia (Atampa rahma) mara kumi)) [Muslim]

Mpya - Maswali

Kuhusu  Maswali Na Majibu Yenu

Kutokana na maswali mengi mno yanayomiminika kila siku kwetu, imekuwa vigumu kutekeleza kazi zake kwa sababu ya upungufu wa watendaji wa hizi kazi. Hivyo Tunasikitika kuwajulisha kwamba kuanzia  tarehe 17 May 2009, tunasimamisha kupokea maswali ili tumalize kwanza ya zamani ambayo ni mengi mno, na yaliyokuwa tayari majibu yake ila hatukujaaliwa kuwatumia katika anuani zenu. Tunasikitika kwa hali ngumu hii ilivyokuwa ambayo imetushinda nguvu, na tunawaomba radhi na mvute subira na kutuombea Allaah Atusahilishie na Atutakabalie. 

Ndugu Zenu

AL HIDAAYA

 

Mpya Mapishi