Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):
Hikma Zake
03-Kuwaridhisha Washirikina Wa Makkah Katika Mkataba Wa Swulhu-Hudaybiyyah
Alhidaaya.com
Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّم) alielekea Makkah pamoja na Swahaba zake (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمْ) kwa ajili ya kutekeleza ‘Umrah, walipofika karibu na Makkah eneo la Hudaybiyyah, ma-Quraysh wa Makkah waliwagomea kungia Makkah, ikawa ni mtihani kwa Waumini, walikaribia kutaka kupigana vita nao! Hatimaye ikabidi kuweko na Sulhu baina yao. Katika kuandika mkataba baina yao, Suhayl ambaye ni katika washirikina wa Makkah akaja hapo na ikawa kama ifuatavyo:
Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamwita mwandishi wake na kumwambia aandike:
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ
BismiLLaahir-Rahmaanir-Rahiym.
Suhayl akasema: Ama Ar-Rahmaan, Wa-Allaahi, hilo silijui lina maana gani, lakini andika:
بِاسْمِكَ اللَّهُمَّ
Bismika Allaahumma
kama ulivyokuwa unaandika nyuma. Waislaam wakapinga na kusema: Wa-Allaahi, hatuandiki ila kwa
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ
Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) (akawakatalia) akasema (kumwambia mwandishi wake) “Andika
بِاسْمِكَ اللَّهُمَّ
Kisha akasema:
“Huu ni mkataba wa Suluhu ambao Muhammad Rasuli wa Allaah ameufikia”.
Suhayl (akapinga) na kusema: Wa-Allaahi, lau tungelijua na kukutambua kuwa wewe ni Rasuli wa Allaah, basi tusingekuzuilia na Al-Ka’bah wala tusingekupiga vita. Lakini andika:
مُحَمَّدُ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ
Muhammad bin ‘Abdillaah.
Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Wa-Allaahi, hakika mimi bila shaka ni Rasuli wa Allaah hata mkinikadhibisha.”
Akamwambia mwandishi aandike:
مُحَمَّدُ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ
Muhammad bin ‘Abdillaah
Waumini wakaghadhibika mno, lakini Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّم) kwa hikmah yake, alikubali iandikwe vile vile walivyotaka washirikina wa Makkah ingawa lilikuwa ni jambo gumu na la ajabu kwa Waumini kuwaridhisha washirikina wa Makkah, ilhali wao walikuwa katika haki. Mkataba ukaandaliwa lakini hatimaye...