Skip navigation.
Home kabah

Faida Mbali Mbali Kuhusu Mwezi Mtukufu Wa Ramadhaan

 
Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh,

Ndugu wapenzi,

Tuna furaha kuwajulisha kuwa tumewaandalia faida mbali mbali muhimu kuhusu Mwezi Mtukufu wa Ramadhaan.   

Nasiha Ya Ijumaa

Nyakati Tatu Muhimu Za Kufanya Ibada – Zisikupite Katika Ramadhaan-

Nyakati tatu hizi ni muhimu sana za kufanya ibada kutokana na fadhila zake kuu. Mwenye kupenda kuchuma thawabu nyingi asizikose khaswa katika mwezi huu Mtukufu Wa Ramadhaan ambao ni mwezi wenye malipo maradufu

1-Wakati wa mwanzo:  Baina ya Alfajiri na jua kuchomoza:

Usimulizi uliothibiti kutoka katika Swahiyh Muslim (564/1) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba walikuwa wakibakia macho wakati huo hadi jua kuchomoza kwani ni wakati mja anapogaiwa rizki yake, na ni wakati wenye kheri nyingi, unampa siha nzuri ya mwili binaadamu, na kwa ujumla ni wakati wenye baraka nyingi za kila aina kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliomba:  

اللهم بارك لأمتي في بكورها  الترمذي, أحمد, أبي داود, ابن ماجه

 

Mpya - Maswali

OMBI JIPYA KUHUSU MASWALI YENU

KWANZA: Tunawaomba muwe na subira baada ya kutuma Maswali yenu, kwani maswali mengi mno yanamiminika humu na wengine wanatuma maswali yao zaidi ya mara tatu kukumbusha. Tunaomba mtambue kwamba maswali yanajibiwa kwa zamu ili kufanya haki katika kuyajibu. 
PILI:  Wanaotuma Maswali ya Mirathi, tunawaomba waweke maelezo kamili kuhusu warithi waliobakia. Watajwe wote wanaohusika kupata urithi  ili maswali yaweze kujibiwa ipasavyo bila ya kukurudishieni barua kukuulizeni.   TATU:  Maswali yawekwe maudhui iliyo wazi ili iwe wepesi kufuatilia na kila swali litumwe katika barua ya pekee.
Tunatumai kupata ushirikiano wenu mwema ili mtufanyie wepesi hizi kazi  ambazo ni nyingi sana  khaswa  za Maswali  na watendaji ni wachache sana.
 
Jazaakum Allaahu Khayra.