Skip navigation.
Home kabah

Nasiha Ya Ijumaa

'Amali Za Kutenda Na Ya Kujiepusha Nayo Katika Mwezi Mtukufu Wa Rajab

AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Kutupa umri hadi kutufikisha mwezi mtukufu wa Rajab ambao ni fursa kwetu kutenda mema yatakayotuchumia thawabu nyingi kuliko miezi mingine. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla ya siku hii kufika. Siku ambayo hakuna mmoja wetu yeyote atakayeweza kuikwepa. Basi hebu kila mmoja wetu ajiulize: "Nimetanguliza nini kwa ajili ya siku hiyo?" Siku ambayo safari yake ni ndefu mno. Vyovyote tutakavyobeba kama ni zawadi huko Aakhirah, hazitoshi wala hatuna hakika nazo kama zitapendekezeka au zitakuwa na thamani huko tuendako ambako kuna makazi ya milele tusiyokuwa na hakika nayo; ima moto au Pepo.   

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

(( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ)) 

 

((Enyi mlioamini! Mcheni Allaah, na kila nafsi iangalie inayoyatanguliza kwa ajili ya Kesho. Na mcheni Allaah, Hakika Allaah, Anazo khabari ya mnayoyatenda)) [Al-Hashr: 18].

Mpya - Maswali

TUNASIKITIKA HATUWEZI KUPOKEA MASWALI KWA SASA. Maswali mengi yanayoulizwa  yameshajibiwa, hivyo tafuta hapo juu ilipoandikwa: "Tafuta Ndani Ya  Alhidaaya"  kwa kuandika  maneno  mawili-matatu yanayohusiana na Swali lako yatajitokeza majibu yake.