Mja Mwema Hafanyi Mijadala
Imaam 'Abdul-Kariym Al-Jazariy amesema:
"Mchaji Allaah hafanyi mijadala."
[Ash-Shu'ab, 8129]
Haytham bin Jamiyl aliulizwa: "Mtu ana ujuzi wa mas-alah ya Sunnah, je, anaweza kufanya mijadala au malumbano katika fani hiyo?" Akajibu: "Hapana, bali anapaswa kuwajulisha watu waijue Sunnah, na wakiipokea kutoka kwake ni vizuri, la wasipoipokea, basi anyamaze (asilumbane)."
[Jaami' Al-Bayaan Al-'Ilm Wa Fadhwlihi, 4/94]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/201
[2] http://www.alhidaaya.com
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F6943&title=Imaam%20%27Abdul-Kariym%20Al-Jazariy%20-%20Mja%20Mwema%20Hafanyi%20Mijadala