Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
03-Zuhd Yake:
Akiomba Du’aa Ya Kujaaliwa Rizqi Ya Kumtosheleza Tu
Alhidaaya.com [1]
Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akimuomba Allaah (سبحانه وتعالى) rizki ya kumtosheleza tu basi akiomba du’aa:
اللَّهُمَّ اجْعَلْ رِزْقَ آلِ مُحَمَّدٍ قُوتًا
Ee Allaah ijaalie rizki ya Ahl wa Muhammad iwe ya kutosheleza tu.” [Muslim]
Na akataja katika Hadiyth yanayompasa bin Aadam kutosheka nayo:
عن أَبي عمرو ، ويقالُ : أَبو عبدِ الله ، ويقالُ : أَبو ليلى عثمان بن عفان رضي الله عنه : أنَّ النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَيْسَ لاِبْنِ آدَمَ حَقٌّ في سِوَى هذِهِ الخِصَالِ : بَيْتٌ يَسْكُنُهُ ، وَثَوْبٌ يُوارِي عَوْرَتَهُ ، وَجِلْفُ الخُبز وَالماء )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu 'Amru (رضي الله عنه) Inasemwa ni Abu 'Abdillaah, na inasemwa Abu Laylaa 'Uthmaan bin 'Affaan (رضي الله عنه) kuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: "Bin Aadam hana haki ya kuwa na zaidi ya vitu aina tatu: nyumba atakayoishi, na mavazi ya kusitiri uchi wake na kipande cha mkate na maji." [At-Tirmidhy, na akasema ni Hadiyth Swahiyh]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10374&title=03-Sifa%20Na%20Akhlaaq%20Za%20Nabiy%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%3A%20Zuhd%20Yake%3A%20Akiomba%20Du%E2%80%99aa%20Ya%20Kujaaliwa%20Rizqi%20Ya%20Kumtosheleza%20Tu