Hadiyth: Husnul-Khuluq (Tabia Njema)
Hadiyth Ya 7
Husnul-Khuluq Ni Sababu Ya Kuingizwa Jannah
Alhidaaya.com [1]
عن أَبِي هُرَيْرَةَ: سُئِلَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم: مَا أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ الْجَنَّةَ؟ قَالَ: ((تَقْوَى اللهِ، وَحُسْنُ الْخُلُقِ)) قَالَ: وَمَا أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ النَّارَ؟ قَالَ: ((الأَجْوَفَانِ: الْفَمُ وَالْفَرْجُ.))
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa: “Jambo gani zaidi litakalokuwa ni sababu ya kumwingiza mtu Jannah?” Akasema: ((Taqwa (kumcha Allaah) na Husnul-Khuluq (tabia njema)). Na akulizwa: “Jambo gani zaidi litakalokuwa ni sababu ya kumwingiza mtu Motoni?” Akasema; ((Mdomo na sehemu za siri)) [Al-Adab Al-Mufrad, Swahiyh Ibn Maajah (3443)], Swahiyh At-At-Tirmidhiy (2004)]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10862&title=07-Hadiyth%20Husnul-Khuluq%3A%20Husnul-Khuluq%20Ni%20Sababu%20Ya%20Kuingizwa%20Jannah