Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu
Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.
Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com [1]
12-Dhambi gani kubwa zaidi?
Dhambi kubwa kabisa ni kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).
يَا بُنَيَّ لَا تُشْرِكْ بِاللَّـهِ ۖ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ ﴿١٣﴾
“Ee mwanangu! Usimshirikishe Allaah, hakika shirki ni dhulma kubwa mno!” [Luqmaan: 13]
سُئِلَ صلى الله عليه وسلم أيُّ الذَّنب أعظم؟ قَالَ: ((أَنْ تدعو للهِ ندّاً وَهُوَ خَلَقَك)) رواه مسلم
Aliulizwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) dhambi gani kubwa? Akasema: ((Ni kumuomba Allaah pamoja na mshirika Na hali Yeye Ndiye Aliyekuumba)) [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7770&title=12-Mukhtasari%20Aqiydah%20Ya%20Muislamu%3A%20Dhambi%20gani%20kubwa%20zaidi%3F