Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu
Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.
Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com [1]
22-Je, Inajuzu kuomba msaada kwa walio hai?
Naam, inajuzu kuomba msaada kwa walio hai katika mambo ambayo wana uwezo nayo.
وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ
Shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na uadui [Al-Maaidah: 2]
((واللهُ فِي عَوْنِ الْعَبْد مَا دام الْعَبْدُ فِي عَوْنِ أخِيه)) رواه مسلم
((Allaah Yuko katika kumsaidia mja Wake maadam mja huyo yuko katika kumsaidia nduguye)) [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7781&title=22-Mukhtasari%20Aqiydah%20Ya%20Muislamu%3A%20Je%2C%20Inajuzu%20kuomba%20msaada%20kwa%20walio%20hai%3F