Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu
Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.
Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com [1]
37-Je, Unahitaji kumuomba Allaah kumtegemea kiumbe yeyote?
Hapana! Huhitaji kumtegemea kiumbe mwengine unapomuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)
وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ
Na watakapokuuliza waja Wangu (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu (kwa ujuzi); Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. [Al-Baqarah: 186]
((إِنَّكُمْ تَدْعُونَ سَمِيعًا قَرِيبًا وَهُوَ مَعَكُمْ)) رواه مسلم
((Hakika nyinyi mnamuomba Mwenye kusikia, Aliye karibu (nanyi) Naye Yuko na pamoja nanyi [kwa ujuzi Wake])) [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7797&title=37-Mukhtasari%20Aqiydah%20Ya%20Muislamu%3A%20Je%2C%20Unahitaji%20kumuomba%20Allaah%20kumtegemea%20kiumbe%20yeyote%3F