Mlango Wa 47
بَابٌ اِحْتِرَامُ أَسْمَاءِ اللَّهِ تَعَالَى وَتَغْيِيرُ الِاسْمِ لِأَجْلِ ذَلِكَ
Kuheshimu Majina Ya Allaah Ta’aalaa Na Kubadilisha Jina Lake Mtu Kwa Ajili Hiyo
عَنْ أَبِي شُرَيْحٍ: أَنَّهُ كَانَ يُكَنَّى: أَبَا الْحَكَمِ. فَقَالَ لَهُ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْحَكَمُ وَإِلَيْهِ الْحُكْمُ)) فَقَالَ: إِنَّ قَوْمِي إِذَا اِخْتَلَفُوا فِي شَيْءٍ أَتَوْنِي فَحَكَمْتُ بَيْنَهُمْ فَرَضِي كِلا الْفَرِيقَيْنِ فَقَالَ: ((مَا أَحْسَنَ هَذَا، فَمَا لَكَ مِنَ الْوَلَدِ؟)) قُلْتُ: شُرَيْحٌ وَمُسْلِمٌ وَعَبْدُ اللَّهِ. قَالَ: ((فَمَنْ أَكْبَرُهُمْ؟)) قُلْتُ: شُرَيْحٌ. قَالَ: ((فَأَنْتَ أَبُو شُرَيْحٍ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَغَيْرُهُ
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Shurayh(رضي الله عنه) kwamba: alikuwa akiitwa Abuu Al-Hakam. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: ((Hakika Allaah ndiye Hakimu na Kwake kuna hukmu zote)) Akasema: Hakika watu wangu wanapokhitilafiana katika jambo, hunijia kisha nikawahukumu baina yao, hapo pande mbili zote zinaridhika. Akasema: ((Uzuri ulioje huo! Je, unao watoto?)) Nikajibu: [Ndio] Shurayh na Muslim na ‘Abdullaah. Akauliza: ((Nani mkubwa wao?)) Nikasema: Shurayh. Akasema: ((Basi wewe ni Abuu Shurayh)) [Abuu Daawuwd na wengineo].
Masuala Muhimu Yaliyomo:
1-Kuheshimu Majina na Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) japokuwa maana yake halisi haikukusudiwa kujisifia nayo (na Abuu Shurayh)
2-Mtu kubadili jina lake kwa ajili hiyo.
3-Kutumia jina la mtoto mkubwa kwa ajili ya kun-yah.
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7903&title=47-Kitaab%20At-Tawhiyd%3A%20Kuheshimu%20Majina%20Ya%20Allaah%20Na%20Kubadilisha%20Jina%20Lake%20Mtu%20Kwa%20Ajili%20Hiyo