Mlango Wa 61
بَابٌ مَا جَاءَ فِي الْمُصَوِّرِينَ
Wachoraji Picha Za Viumbe Wachongaji Masanamu Vinyago n.k.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((قَالَ اللهُ تَعَالَى: وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنْ ذَهَبَ يَخْلُقُ كَخَلْقِي؛ فَلْيَخْلُقُوا ذَرَّةً، أَوْ لِيَخْلُقُوا حَبَّةً، أَوْ لِيَخْلُقُوا شَعِيْرَةً )) أَخْرَجَاهُ
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Aliyetukuka Amesema: Nani dhalimu zaidi kuliko anayejaribu kuumba kama kuumba Kwangu? Basi na waumbe chembe moja au waumbe punje ya nafaka, au waumbe chembe ya shayiri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
وَلَهُمَا عَنْ عَائِشَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) قَال: ((أَشَدُّ النَّاسِ عَذَابًا يَوْمَ القِيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهِئُونَ بِخَلْقِ اللَّهِ))
Nao (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watakaokuwa na adhabu kali Siku ya Qiyaamah ni wanaomuiga Allaah katika uumbaji Wake))
وَلَهُمَا عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) : سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((كُلُّ مُصَوِّرٍ فِي النَّارِ يُجْعَلُ لَهُ بِكُلِّ صُورَةٍ صَوَّرَهَا نَفْسٌ يُعَذَّبُ بِهَا فِي جَهَنَّمَ))
Nao (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kila mchoraji picha atakuwa motoni. Kila picha aliyoichora, itatiwa roho nayo itamuadhibu katika Jahannam))
وَلَهُمَا عَنْهُ مَرْفُوعًا: ((مَنْ صَوَّرَ صُورَةً فِي الدُّنْيَا كُلِّفَ أَنْ يَنْفُخَ فِيهَا الرُّوحَ وَلَيْسَ بِنَافِخٍ))
Nao (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia kutoka kwake pia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) Hadiyth Marfuw’: ((Atakayechora picha duniani atalazimishwa aitie roho (Siku ya Qiyaamah), na wala hatoweza))
وَلِمُسْلِمٍ عَنْ أَبِي الهَيَّاجِ قَالَ: قَالَ لِي عَلِيٌّ: أَلاَ أَبْعَثُكَ عَلَى مَا بَعَثَنِي عَلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)؟: أَلاَّ تَدَعَ صُورَةً إِلاَّ طَمَسْتَهَا وَلاَ قَبْرًا مُشْرِفًا إِلاَّ سَوَّيْتَهُ
Na Muslim amesimulia kutoka kwa Abuu Al-Hayyaaj amesema: ‘Aliyy ameniambia: “Je, nikutume lile alilonituma Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)? Kwamba: Usibakishe sura (picha, sanamu, kinyago) yoyote ila uiharibu, wala kaburi lilonyanyuliwa ila (ulibomoe na) ulisawazishe.”
Masuala Muhimu Yaliyomo:
1-Karipio kali kwa wenye kuchora (na kutengeneza, kuchonga) picha, masanamu, vinyago n.k.
2-Imekaripiwa vikali kwa sababu watengenezaji na wachoraji picha hawamuheshimu vilivyo Allaah (سبحانه وتعالى) kama Alivyosema Yeye Mwenyewe: ((Nani dhalimu zaidi kuliko anayejaribu kuumba kama kuumba Kwangu?)).
3-Tanbihi ya nguvu kutofuatisha uwezo wa Allaah (سبحانه وتعالى) katika kuumba na ule wa wengine kama unavyoashiria katika kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى): ((Basi na waumbe chembe moja au waumbe punje ya nafaka, au waumbe chembe ya shayiri)).
4-Tangazo kuwa wachoraji, watengenezaji picha wataadhibiwa vikali zaidi (Siku ya Qiyaamah).
5-Allaah (سبحانه وتعالى) Ataumba roho katika kila picha (sanamu, kinyago n.k.) nayo itamuadhibu mwenye kuzitengeneza katika moto wa Jahannam.
6-Wafanya picha wataambiwa wazitie roho (uhai) picha zao.
7-Amri ya kuziharibu picha, vinyago, masanamu n.k. popote zitakapoonekana. (Pia kusawazisha makaburi yaliyonyanyuliwa).
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7917&title=61-Kitaab%20At-Tawhiyd%3A%20Wachoraji%20Picha%20Za%20Viumbe%20Wachongaji%20Masanamu%20Vinyago%20n.k.