SWALI:
swali: kwa mwanamume aliye safari akaacha mkewe kwa muda wa miaka miwili au zaidi, mke anapokuwa na hisia za kimapenzi anatakiwa kufanya nini na mumewe hayupo?
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kuwa mbali na mumeo ambaye yuko safarini. Hakika hili ni tatizo sugu katika jamii yetu kwa wanawake kuachwa kwa muda mrefu ikiwa mume yuko katika kutafuta maisha kwa ajili ya familia yake.
Tatizo hili haliwezi kutatuliwa bila Imani ya nguvu kwani bila hivyo matamanio yanakuja kwa haraka kwa mwanamke na inabidi apate cha kumtuliza ili aone wepesi wa moyo na mwili. Imani ya Muislamu huzidi na kupungua kutegemea na mambo mengi katika maisha yake. Allaah Aliyetukuka Anasema: “Hakika Waumini ni wale ambao anapotajwa Allaah nyoyo zao hujaa khofu, na wanapo somewa Aayah Zake huwazidisha Imani, na wakamtegemea Mola wao. Hao ambao wanashika Swalaah na wanatoa katika yale tunayowaruzuku” (al-Anfaal [8]: 2 – 3).
Kwa hali hiyo, mwanamke au mwanamme ambaye anataka kujitenga na uchu wake ni muhimu afanye mambo yafuatayo:
Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Atuhafadhi sote na kumuasi hapa duniani ili Atuingishe Peponi Kesho Akhera na Atulinde na madhambi hapa ulimwenguni.
Na Allaah Anajua zaidi.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/67
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F4684&title=Mume%20Anapokuwa%20Safarini%20Kwa%20Muda%2C%20Mke%20Afanyeje%20Abakie%20Katika%20Taqwa%20Na%20Stara%3F