Achari Ya Papai Bichi Embe Karoti Sambharo
Vipimo
Papai bichi katakata vipande vyembamba – 1
Embe mbichi, menya na katakata slice - 3
Karoti kataka vipande virefurefu - 2
Pilipili mbichi kubwa za kijani na nyekundu, kata katikati kwa urefu - Mteko wa mkono
Hardali/Rai (mustard seeds) - 1 kijiko cha supu
Majani ya mchuzi/mvuje (curry patta) - Kiasi
Mvuje wa unga (asafoetida) - 2 vijiko cha chai
Mafuta - ½ kikombe
Ndimu – kamua - 3
Siki - ¼ kikombe
Chumvi - Kisia
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Weka hardali/rai na majani ya mchuzi, kaanga kidogo vitoe harufu
Tia mchanganyiko wa papai, embe, karoti na pilipili
Tia chumvi, mvuje wa unga, kaanga dakika kama 3 -4 tu. Usipike mpaka vikaiva.
Tia ndimu na siki, ondosha katika moto kisha jaza katika chombo au chupa za kuwekea achari.
Kidokezo:
Mvuje wa unga (asafoetida) unauzwa tayari katika vichupa vidogo au saga mwenyewe nyumbani
asafoetida
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/146
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7205&title=Achari%20Ya%20Papai%20Bichi%20Embe%20Karoti%20%20%28India%20Sambharo%29