Alhidaaya.com
Published on Alhidaaya.com (https://www.alhidaaya.com/sw)

Ukurasa Wa Kwanza > Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Fadhila Zake Mbalimbali > 48-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

48-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

 

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

48-Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

 

www.alhidaaya.com [1]

 

 

 

عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ يَوْمًا فَصَلَّى عَلَى أَهْلِ أُحُدٍ صَلاَتَهُ عَلَى الْمَيِّتِ، ثُمَّ انْصَرَفَ إِلَى الْمِنْبَرِ فَقَالَ ‏ "‏ إِنِّي فَرَطٌ لَكُمْ، وَأَنَا شَهِيدٌ عَلَيْكُمْ، وَإِنِّي وَاللَّهِ لأَنْظُرُ إِلَى حَوْضِي الآنَ، وَإِنِّي أُعْطِيتُ مَفَاتِيحَ خَزَائِنِ الأَرْضِ ـ أَوْ مَفَاتِيحَ الأَرْضِ ـ وَإِنِّي وَاللَّهِ مَا أَخَافُ عَلَيْكُمْ أَنْ تُشْرِكُوا بَعْدِي، وَلَكِنْ أَخَافُ عَلَيْكُمْ أَنْ تَنَافَسُوا فِيهَا ‏"‏‏.‏

 

Kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) amesema: Siku moja Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikwenda nje na akaongoza Swalaah za maiti; Mashuhadaa wa Uhd, kisha akapanda katika Minbar akasema: “Mimi nitaandaa njia kwa ajili yenu kama muasisi na nitakuwa Shahidi kwa ajili yenu. Na wa-Allaahi, ninaiona Al-Hawdhw (chemchemi ya Al-Kawthar) sasa hivi na nimepewa funguo za hazina zote za ardhi (au funguo za ardhi). Na Wa-Allaahi, hakika mimi sikhofu kuwa mtamshirikisha Allaah baada ya kufa kwangu, lakini nakhofu kuwa mtagombana baina yenu kwa ajili ya vitu vya kidunia.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Kupewa Hazina Za Ulimwengu: Ni kuongezeka na kupanuka Uislamu, na kujaaliwa ushindi mkubwa na mateka ya mali, kwa sababu unapopatikana ushindi wa nchi ni sawa na kumiliki mali na hazina zake.

 

 

Share [2]
www.alhidaaya.com

Source URL: https://www.alhidaaya.com/sw/node/10296

Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10296&title=48-Fadhila%20Za%20Nabiy%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%3A%20Amepewa%20Funguo%20Za%20Hazina%20Za%20Ulimwengu%20Wote